ASKOFU wa Jimbo Katoliki la Tanga, Mhashamu Anthony Banzi amesema iwapo Serikali inataka nchi ya viwanda hawana budi kuweka msukumo mkubwa kwenye kupiga vita dawa za kulevya vitendo ambazo zimechangia kwa asilimia kuwaharibu vijana wengi hapa nchini. 

Banzi aliyasema hayo wakati wa uzinduzi wa Juma la Elimu wilaya ya Tanga ambapo kiwilaya lilifanyika kwenye shule ya Sekondari Tanga Don Bosco iliyopo eneo la Maweni jijini Tanga inayomilikiwa na Kanisa Katoliki Jimbo la Tanga. 

Alisema ili kutimiza azma hiyo ambayo ni muhimu kwa ukuaji wa uchumi wa nchi lazima kuwepo na juhudi kubwa za kuuteketeza mtandao wa dawa za kulevya hapa nchini uliyoharibu vijana wengi ambao wangekuwa nguvu kazi kubwa ya Taifa la kesho. 

“Kama tunataka kuifanya nchi kuwa ya viwanda maana yake kila mmoja apate elimu ya madhara ya dawa za kulevya lengo kubwa likiwa kuliondoa tatizo hilo kwa vijana ambalo limekuwa likipoteza nguvu kazi ambayo ingeweza kutumika katika shughuli mbalimbali lakini pia kuwepo kwa mapambano ya kupiga vita hali hiyo “Alisema. 

ASKOFU wa Jimbo Katoliki la Tanga, Mhashamu Anthony Banzi akizungumza na wanafunzi kutoka shule mbalimbali Jijini Tanga wakati wa uzinduzi wa Juma la Elimu wilaya ya Tanga ambapo kiwilaya lilifanyika kwenye shule ya Sekondari Tanga Don Bosco iliyopo eneo la Maweni jijini Tanga inayomilikiwa na Kanisa Katoliki Jimbo la Tanga.
ASKOFU wa Jimbo Katoliki la Tanga, Mhashamu Anthony Banzi wa pili kulia  akimkiliza mwanafunzi wa kidato cha nne katika shule hiyo wakati alipokuwa akifafanua jambo
ASKOFU wa Jimbo Katoliki la Tanga, Mhashamu Anthony Banzi katikati akionyesha jambo na Sista ambaye anafanya kazi kwenye shule hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...