Na Lorietha Laurence.

Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe amezindua Vifaa vya kufundishia vyenye thamani ya shilling 100 kwa ajili ya Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo(TaSUBa) vitavyowawezesha wanafunzi kujifunza kwa vitendo namna ya kutengeneza picha jongefu.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo leo Wilayani Bagamoyo, Dkt.Mwakyembe amesema kuwa vifaa hivyo ni muhimu katika maendeleo ya kitaaluma ya wanafunzi wa Taasisi hiyo katika kuwaongezea ujuzi katika vitendo na baadaye kuwa watendaji bora na makini.

“Vifaa hivi ni tija katika kuhakikisha kuwa wanafunzi wanajifunza kwa vitendo na hivyo kuzalisha watu wenye taaluma zenye tija na zenya kuleta matokeo chanya kwa ajili ya maendeleo nchi”alisema Mhe.Dkt.Mwakyembe.

Aliongeza kwa kuhaidi kuwa atahakikisha viongozi mbalimbali wakiwemo Mawaziri na Mabalozi wanapata fursa ya kuitembelea TaSUBa ili wajionee kwa macho hazina kubwa waliyonayo katika kukuza na kuendeleza sanaa na utamaduni.


Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe akizindua rasmi vifaa vya Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBA), 4 Aprili, 2017 Wilayani Bagamoyo Mkoani Pwani.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe akipokea zawadi za picha za kuchora toka kwa Mkurugenzi wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBA), Dkt. Herbet Makoye wakati alipowasili katika taasisi hiyo kuzindua vitendea kazi vya taasisi hiyo 4 Aprili, 2017 Wilayani Bagamoyo Mkoani Pwani.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (mwenye tai nyekundu) akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni (TaSUBA) pamoja na watendaji wengine wa Wizara mara baada ya kuzindua vitendea kazi vya taasisi hiyo 4 Aprili, 2017 Wilayani Bagamoyo Mkoani Pwani.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (mwenye tai nyekundu) akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni (TaSUBA), Watendaji waWizara pamoja na wageni toka nje ya nchi mara baada ya kuzindua vitendea kazi vya taasisi hiyo 4 Aprili, 2017 Wilayani Bagamoyo Mkoani Pwani. 
(PICHA ZOTE NA BENEDICT LIWENGA-WHUSM).



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...