Na Mwandishi Wetu, Chalinze

TAASISI ya Kifedha ya Bayport Financial Services, jana iliikomboa Halmashauri mpya ya wilaya Chalinze kwa kuipatia kompyuta mbili kwa ajili ya kupunguza changamoto za upungufu wa vifaa vya kiutendaji, ikiwa ni miezi michache tangu kuanzishwa kwa Halmashauri hiyo mpya.

Kompyuta hizo zilipokewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Edes Lukoa katika ofisi yake, ikiwa na lengo la kuhakikisha kuwa Halmashauri hiyo inatimiza wajibu wake wa kuwatumikia wana Chalinze na Watanzania kwa ujumla kwa kutumia kompyuta hizo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Chalinze Edes Lukoa akipokea kompyuta mbili kutoka kwa Taasisi ya Bayport Financial Services ikiwakilishwa na Mratibu wa Masoko Mercy Mgongolwa.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri mpya ya Chalinze mkoani Pwani, Edes Lukoa mwenye koti jeusi, akipokea msaada wa kompyuta mbili kutoka kwa Mratibu wa Masoko wa Bayport Fiancial Services, Mercy Mgongolwa. Wanaoshuhudia ni Meneja wa Kanda ya Kati Christopher Kihwele kushoto kwa Mercy na Meneja wa wa Bayport Bagamoyo Francis Sumila na Katibu wa Mbunge wa Chalinze Ridhiwan Kikwete Idd Swala kulia kwa Mkurugenzi wa Chalinze.

Akizungumza jana katika makabidhiano hayo wilayani Chalinze, Mratibu wa Masoko wa Bayport Financial Services, Mercy Mgongolwa, alisema kwamba lengo la kuipatia kompyuta hizo linatokana na dhamira ya kuona wilaya hiyo inasonga mbele kimaendeleo.

Alisema kugawa kompyuta hizo ni mwendelezo wa nia yao baada ya kuzindua ugawaji wa kompyuta hizo 205 zilizoanza kusambazwa katika ofisi mbalimbali za serikali baada ya kuzinduliwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angellah Kairuki.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...