NA IS-HAKA OMAR, ZANZIBAR.

ZAIDI ya Nyumba 300 katika maeneo mbali mbali ya Mkoa wa Mjini Magharibi zimeathiriwa na Mvua za masika zinazoendelea kunyesha hivi sasa.

Akizungumza katika mtaa wa ziwa maboga sheha wa shehia ya Tomondo, Bw. Mohamed Omar Said alisema zaidi ya nyumba 200 katika eneo hilo zimeathiriwa na mvua kwa kujaa maji na zingine kuporomoka.

Bw. Said alifafanua kwamba baadhi ya wakaazi wa eneo hilo wamehama katika makaazi yao na kuomba hifadhi katika maeneo mengine yaliyokuwa salama, huku idadi ya nyumba zinazoathiriwa na mvua hizo zikiendelea kuongezeka kadri mvua zinavyioendelea kunyenyesha.

Mbali na maeneo hayo pia katika mitaa ya Meli nne, Fuoni janga mizini na Fuoni Migombani kuna nyumba zaidi ya 100 zimeathiriwa na mvua hizo.

Akizungumza juu ya athari hizo, Mjumbe wa sheha wa shehia ya kibondeni, Bi. Zuhura Ame alisema hali za baadhi ya wananchi waliopata maafa hayo sio nzuri hivyo wanahitaji msaada wa dharura.

Alisema kwamba licha ya viongozi wa majimbo hasa Wabunge, wawakilishi na madini baadhi yao tayari wameanza kutoa msaada na wengine ndio wanajipanga kufika kwa ajiri ya kuwafariji wananchi lakini bado panahitajika nguvu za pamoja baina ya wananchi, vyama vya kisiasa na serikali ili kuinusuru nchi kuingia katika maafa makubwa.

Naibu katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dkt. Abdalla Juma akipokea maelezo kutoka kwa viongozi wa mtaa akiwemo sheha wa shehia ya Tomondo, Mohamed Omar katika eneo la Ziwa maboga ambapo zaidi ya nyumba 200 zimeathiriwa na mvua za masika zinazoendelea kunyesha. 
Nyumba mbali mbali zilizoathiriwa na maji ya mvua katika eneo la Tomondo Wilaya ya Magharibi “B” Unguja.  
Katibu wa Tawi la CCM Tomondo, Hassan Kipanga Abdalla akimweleza Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar hali ya waakazi wa shehia hiyo kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha hivi sasa. 
Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dkt.Abdalla Juma Saadala akiwafariji wananchi wa eneo la Mwanakwerekwe Meli nne, waliopata maafa kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha hivi sasa. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...