Mwenyekiti wa Chama cha Wanasheria Wanawake Nchini Tanzania TAWLA Bi. Athanasia Soka akikata keki pamoja na baadhi ya wanachama wa chama hicho katika hafla fupi ya chama hicho kutimiza miaka 27 tamgu kilipoanzanishwa baada ya kusajiliwa rasmi mwaka 1990 na kuanza kazi zake rasmi hapa nchini. 

Chama hicho kimefanikiwa kuanzisha matawi yake katika mikoa ya Tanga, Dodoma, Arusha, Mwanza pamoja na Dar es salaam na chama hicho kimeweza kusaidia mamilioni ya watanzania hasa wanawake katika masuala ya msaada wa kisheria katika unyanyasaji wa kijinsia na migogoro ya kifamili hasa ndoa na masuala mengine, hafla hiyo iliyofanyika ofisi za taasisi hiyo Ilala Bungoni
Mwenyekiti wa Chama cha Wanasheria Wanawake Nchini Tanzania TAWLA Bi. Athanasia Soka akimlisha keki Mwanachama wa chama hicho Bi Mariam Mvano wakati wa hafla hiyo.
Mwenyekiti wa Chama cha Wanasheria Wanawake Nchini Tanzania TAWLA Bi. Athanasia Soka akizungumza na wanachama hao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...