Katika kuazimisha siku ya mama duniani Efm redio kupitia kipindi chake cha uhondo wametoa zawadi kwa wakina mama wa wasikilizaji wao katika tafrija fupi iliopewa jina la “Begi la mama”.
Tafrija hiyo ilifanyika katika ofisi za efm redio siku ya jana kuanzia saa 6:00 mchana hadi saa 9:00 Alasiri. Begi
la mama lilitolewa kwa wakina mama 15 ambao stori zao ziliandikwa na
watoto wao na kuonekana kugusa mioyo ya wasikilizaji wengi kwa yale
magumu waliopitia.
Mtayarishaji wa kipindi cha uhondo Asha manga akipeleka begi la mama likiwa limejaa zawadi kem kem
Timu nzima ya kipindi cha Uhondo ikiongozwa na Dina Marios wakimtunza mama nguo kutoka katika begi.
Muda wa chakula ukafika.
Mtangazaji wa kipindi cha uhondo akimuhoji mshindi ambae alikuja na mama yake kwaajili ya kuzawadiwa begi hilo.
Mama akiwa kashikilia zawadi alizotunzwa na Efm redio.
Timu
nzima ya kipindi cha uhondo ikiongozwa na Dina Marios mstari wa pili
(wakwanza kushoto) akifatiwa na Sofia Amani, Leah Chambo, Rdj Con
wengine ni Bi, Hindu, Swebe Santana, Asha manga, na wengineo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...