Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii , Jinsia , Wazee na Watoto kwa kushirikiana na Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Japan –JAICA- wametoa mrejesho wa utekelezaji wa mpango wa kuboresha huduma na kutatua matatizo madogo kwa kutumia rasimilimali zilizopo –KAIZEN.
Mbali na kutoa mrejesho huo pia wameipongeza Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa kuboresha utoaji wa huduma.
Mpango huo ambao unahusisha watoa huduma umesaidia watumishi kutoa huduma bora, kuzingatia muda wa utoaji huduma na hivyo kupunguza malalamiko kwa wateja.
'Tumefanya tathimini tumeona jinsi ambavyo mmeboresha utoaji wa huduma na kupunguza mlalamiko kwa wananchi , wauguzi wanahudumia wagonjwa kwa upendo na wanatumia lugha nzuri lakini hata mazingira ya Hospitali ni safi’’ amesema Noriyuki Miyamoto.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Utumishi wa MNH Bwana Makwaia Makani amesema tangu kuanza kutekelezwa kwa mpango huo mwaka 2008 kumekua na mabadiliko mengi hospitalini hapo na kusisitiza kuwa hospitali hiyo itahakikisha wananchi wanaendelea kupata huduma bora.
Baadhi
ya wauguzi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili wakimsikiliza Mkurugenzi wa Utumishi
wa MNH Bwana: Makani katika mkutano huo uliofanyika leo.
Bi Rose
Mpayo Muwezeshaji kutoka
Hospitali ya Rufaa Kanda ya Mbeya
akielezea umuhimu wa utoaji huduma bora kwa wateja.
Wauguzi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili wakifuatilia maelezo kutoa kwa mtoa mada.
Mkurugenzi wa
Utumishi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Makwaia Makani akitoa neno kwa
wauguzi wa Hospitali hiyo katika mkutano
wa kupokea mrejesho kuhusu mpango wa kuboresha huduma na kutatua matatizo
madogo kwa kutumia rasilimali
zilizopo-KAIZEN .
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...