Balozi wa Tanzania ndani ya Muungano wa Visiwa vya Komoro, Mhe. Sylvester M. Mabumba tarehe 15 Mei alikabidhi hati zake za uwakilishi kwenda kwa Mhe. Azali Assoumani, Rais wa Muungano wa Visiwa vya Komoro. Hafla ya kukabidhi hati hizo ilifanyika kwenye Ukumbi wa Ikulu ya Komoro ijulikanayo kama  Beit. Wakati akisoma risala yake, Mhe. Balozi alijitambulisha kwa Mhe. Rais na kueleza furaha yake ya kuteuliwa kwake kuwa Balozi wa pili kutoka Tanzania kuja kutumikia nchini Komoro. Aidha, Mhe. Balozi alieleza furaha yake kwa mapokezi mazuri aliyopatiwa tangu kuwasili kwake Visiwani  Komoro ambapo aliongezea kwa kueleza kuwa anajisikia yupo nyumbani. 
Alieleza kuwa anatambua kazi kubwa iliyopo mbele yake na kuahidi kuwa katika kipindi chake wakati akiwa Balozi nchini hapa atajitahidi kukuza mahusiano yaliyopo baina ya Tanzania na Komoro. Sambamba na hilo, Mhe. Balozi alieleza dhamira yake ya kutaka kuona mahusiano baina ya nchi hizi mbili yanakuwa na manufaa kwa pande zote halikadhalika kukua kwa uhusiano wa kindugu kwani mahusiano baina ya Tanzania na Komoro ni ya kihistoria. 
 Akijibu risala hiyo, Mhe. Azali Assoumani, Rais wa Muungano wa Visiwa vya Komoro naye alianza kwa kuonyesha furaha yake ya kuwasili kwa Balozi pamoja na kukiri kupokea barua ya kurejea Balozi aliyepita na kuwasili kwa Balozi wa sasa. Alieleza kuwa kila Mkomoro hujisikia nyumbani pindi anapo tembelea Tanzania kutokana na ukarimu wanao onyeshwa wanapokuwa huko. Aidha Mhe. Rais alimuhakikishia Mhe. Balozi kuwa atarajie kupata ushirikiano wake pamoja na wa Serikali yake katika kipindi chote atakapo kuwa hapa. 
Mhe. Balozi Mabumba alichukua fursa hiyo pia ya kumuomba Mhe. Rais Azali afanye ziara ya kikazi nchini Tanzania ili kuweza kudumisha mahusiano yaliyopo baina ya nchi hizo mbili. 
 Balozi wa Tanzania ndani ya Muungano wa Visiwa vya Komoro, Mhe. Sylvester M. Mabumba akiwasili kwenye Ikulu ya Komoro ijulikanayo kama  Beit tayari kwa kukabidhi hati zake za uwakilishi  kwa Mhe. Azali Assoumani, Rais wa Muungano wa Visiwa vya Komoro.
 Balozi wa Tanzania ndani ya Muungano wa Visiwa vya Komoro, Mhe. Sylvester M. Mabumba akisoma risala yake kwenye Ikulu ya Komoro ijulikanayo kama  Beit kabla ya kukabidhi hati zake za uwakilishi  kwa Mhe. Azali Assoumani, Rais wa Muungano wa Visiwa vya Komoro.
 Balozi wa Tanzania ndani ya Muungano wa Visiwa vya Komoro, Mhe. Sylvester M. Mabumba akikabidhi hati zake za uwakilishi  kwa Mhe. Azali Assoumani, Rais wa Muungano wa Visiwa vya Komoro kwenye Ikulu ya nchi hiyo. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...