Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) anaeziwakilisha nchi 23 za Afrika, Bw. Maxwell Mkwezalamba (wa pili kulia) akieleza kuwa Tanzania inakua kwa kasi kiuchumi jambo ambalo linawavutia viongozi wengi kufuatilia kwa karibu maendeleo yake, alipokutana na Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), (kushoto), katika Ukumbi wa Wizara Jijini Dar es Salaam. 
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), akiongoza Mkutano kati yake na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) anaeziwakilisha nchi 23 za Afrika, Bw. Maxwell Mkwezalamba (mbele kulia) ambapo alisema mahitaji makubwa wa nchi ni maendeleo ya kilimo na upatikanaji wa nishati ya umeme ili viweze kuchochea uchumi wa viwanda. Mkutano huo umefanyika katika Ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), (watatu kushoto) na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) anaeziwakilisha nchi 23 za Afrika, Bw. Maxwell Mkwezalamba (wa tatu kulia) wakiwa katika picha ya pamoja na Viongozi na Maafisa waandamizi wa Wizara hiyo baada ya kumalizika kwa mkutano kuhusu hali ya uchumi katika Ukumbi wa Wizara Jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wajumbe wa Mkutano kati ya Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) anaeziwakilisha nchi 23 za Afrika, Bw. Maxwell Mkwezalamba (hayupo pichani) wakimuaga baada ya kumalizika kwa Mkutano katika ukumbi wa Wizara hiyo Jijini Dar es Salaam.(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-WFM)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...