Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe amesema kuwa timu ya Taifa Stars itafanya vizuri katika mashindano mbalimbali itakayoyakabili  hapo baadae,kutokana na wadau wanavyojitokeza kuiunga mkono.

Mwakyembe ameyasema hayo wakati kishuhudia utiaji saini mkataba kati kampuni ya ya Bia ya Serengeti (SBL) na Shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini (TFF) wenye thamani ya sh.bilioni 2.1,utakaodumu kwa miaka mitatu na  kuifanya SBL kuwa mdhamini mkuu wa timu ya Taifa Stars.

“Kwa niaba ya serikali,tunaishukuru sana kampuni ya SBL kwa kurejea tna kuwa mdhamini mkuu wa Taifa Stars,lakini pia tunatoa wito kwa kampuni zingine na watu binafsi wenye mapenzi na michezo kujitokeza na kutoa michango ya hali na mali ili kuendeleza sekta hiyo hapa nchini”,aliesema Waziri Mwakyembe.

Nae Mkurugenzi Mtendaji wa SBL ,Helene Weesie amesema kuwa SBL imekuwa mdhamini kwa kipindi cha pili baada ya kampuni hiyo kufanya udhamini wa timu ya taifa stars mwaka 2007 hadi 2011.

Amesema timu ya Taifa Stars itakuwa inapokea sh.milioni 700 kila mwaka ambapo itakuwa ni pamoja na kutangaza chapa ya SBL wakati wa mechi za ndani na ugenini zitakazochezwa na timu hiyo.

Kwa upande wa Rais wa TFF, Jamal Malinzi ameishukuru SBL kwa kuunga mkono katika kusaidia maandalizi ya timu ya taifa Stars,akaongeza kusema kuwa udhamini huo utasaidia katika kufanikisha maandalizi mazuri na ushiriki kikamilifu wa timu hiyo katika mashindano mbalimbali, ndani na nje ya nchi.

“Udhamini wa SBL umekuja kwa wakati mwafaka, wakati ambapo timu yetu ya taifa ipo katika hatua za maandalizi kwa mashindano ya kikanda na kimataifa,” alisema Malinzi.

Mkurugenzi Mkuu wa SBL, Helene Weesie (kulia ) akipeana mkono na Rais wa TFF, Jamal Malinzi (kushoto) mara baada ya kukabidhiana
mfano wa hundi ya Sh. Bilioni 2.1,Pichani kati anaeshuhudia tukio hilo ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe.

Mkurugenzi Mkuu wa SBL, Helene Weesie (kushoto) na Rais wa TFF, Jamal Malinzi (kulia) kwa pamoja wakionesha mikataba waliowekeana saini, leo mbele ya Waandishi wa habari,kwenye hafla fupi iliofanyika jioni ya leo jijini Dar.Pichani kati anaeshuhudia tukio hilo ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe.
 

Wakiweka  saini mikataba hiyo.

Pichani kati ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe akizungumza mbele ya Waandishi wa habari mapema leo jioni,kwenye hafla fupi ya uwekaji saini mkataba kati ya kampuni ya ya Bia ya Serengeti (SBL) na Shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini (TFF) wenye thamani ya sh.bilioni 2.1 .

Baadhi ya Waandishi wa Habari na baadhi ya wafanyakazi wa TFF na Wizara wakishuhudi tukio la uwekaji saini mkataba wa udhamini kwa timu ya Taifa Stars wenye thamani ya sh.bilioni 2.1 uliotolewa na kampuni ya SBL  na hatimaye kuifanya kampuni hiyo kuwa mdhamini mkuu wa timu ya Taifa Stars,hafla hiyo imefanyika jioni ya ya leo jijini. Picha na Michuzi Jr.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...