Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

Uongozi wa Klabu ya Simba, umeweka bayana uamuzi wao wa kwenda Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa) kudai haki yao baada ya kupokwa pointi tatu na Kamati ya Katiba, Sheria na Hadhi za Wachezaji huku wakiwa wanasubiri barua kutoka Bodi ya Ligi ili wawasilishe malalamiko yao.

Simba imefikia hatua hiyo baada ya Kamati ya utendaji kukaa na kuamua kwa kauli moja kulipeleka mbele zaidi suala hilo kutokana na kuona kasoro za kikanuni katika maamuzi yaliyotolewa na Kamati ya Uendeshaji wa Usimamizi wa Ligi kwa sababu ambazo wanaziona si za msingi kutokana na kanuni kuwa wazi.

Akizugumza na wanahabari leo Jijini Dar es salaam, Rais wa klabu ya Simba, Evans Aveva, amesema wanachokisubiria kwa sasa ni ku njia zipo nyingi za wao kupata haki yao, hivyo wanasubiri kupewa barua kutoka Bodi ya Ligi ambayo wataiambatanisha kwenda Fifa kudai haki yao.

Aveva amesema wamefuatilia njia za kudai haki yaona wameambiwa gharama inaweza kuanzia dola 15,000 na wapo tayari kulipa ili tupate haki yao ambayo mpaka sasa wanasikia tu kama wamepokwa pointi 3 walizopatiwa na kamati ya saa 72 baada ya kushinda rufaa yao dhidi ya Kagera Sugar ambayo inadaiwa ilimchezesha beki wake, Mohammed Fakhi akiwa na kadi tatu za njano dhidi yao.

Maazimio hayo yaliyofikiwa kwa pamoja na kamati ya utendaji yameainisha kuwa pamoja na hilo, pia wanapeleka malalamiko yao kuhusiana na mchezaji wao Mbaraka Yusuph aliyeidhinishwa kucheza katika klabu ya Kagera wakati tayari akiwa na leseni ya kuchezea ya klabu ya Simkba.

Raisi wa Klabu ya Simba Evance Aveva akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na uamuzi wa kamati ya Utendaji wa klabu hiyo kuazimia kwa pamoja kupeleka malalamiko yao Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani FIFA kutokana na kutokufa nyiwa haki na Shirikisho la Mpiera wa Miguu Nchini TFF.
 Raisi wa Klabu ya Simba Evance Aveva akionesha leseni ya mchezaji Mbaraka Yusuph waliyopatiwa na  Shirikisho la Mpiera wa Miguu Nchini TFF.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...