Sisi watanzania tunaoishi Sweden kwa
majonzi na masikitiko makubwa tunatoa pole zetu kuwafikia familia zilizoguswa
na msiba, shule ya Lucky Vicent Arusha na Taifa kwa ujumla kwa kupoteza watoto,
dereva, na waalimu.
Habari hizi zimetugusa
sana na kuleta simanzi na masikitiko makubwa katika jamii ya Watanzania hapa
Sweden. Tunapendelea pia kuipongeza serikali yetu kwa jitihada zake za
kukabiliana na janga hilo bila kupoteza wakati na pia kuwafariji wafiwa katika
wakati huu mgumu.
TUNATANGULIZA
UPENDO NA MSHIKAMANO KWA TAIFA LETU
KWA
NIABA YA WATANZANIA SWEDEN
MWENYEKITI
NORMAN
JASSON
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...