Na: Frank Shija – MAELEZO 

WADAU mbalimbali wameipongeza Serikali kwa uamuzi wa kuivunja Mamlaka ya Ustawishaji wa Makao Makuu Dodoma (CDA) iliyofikiwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli. 

Wakitoa maoni yao juu ya umauzi huo wa Serikali, wameeleza kuwa kuvunjwa kwa Mamlaka hiyo kumekuja wakati muafaka kwani kutapunguza kero na migogoro ya ardhi iliyokuwa ikiendelea katika Manispaa ya Dodoma. 

Aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Maalum iliyoundwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Jordan Rugimbana,iliyokuwa inashughulikia changamoto za wananchi dhidi ya CDA, Bw. Aron Kinunda alisema kuwa uamuzi huo huko sahihi kwani umekuja wakati muafaka kwa kuzingatia malengo halisi ya uanzishaji wa mamlaka hiyo kuwa yamekamilika kwa asilimia kubwa ukizingatia na mahitaji halisi ya wakati huu. 

“Ni hatua nzuri katika mustakabari wa maendeleo ya Dodoma, kwani sasa migogoro mingi ya ardhi iliyokuwa inatokana na mgongano wa kisheria haitarajiw kujitokeza tena na badala yake Manispaa itajikita katika kuweka mazingira rafiki ya umiliki wa ardhi ikiwemo kuongeza muda wa hati ya umiliki kutoka miaka 33 hadi 99 kama ambavyo maeneo mengine ya nchi yanavyofanya.” Alisema Kinunda. 

Aliongeza kuwa wananchi watakuwa wamefarijika sana kwani walikuwa wanaiona CDA kama adui yao mkubwa ambapo imesababisha malalamiko mengi ya kuchukuliwa ardhi zao bila ya kulipwa fidia na urasimu katika upimaji na utoaji wa hati za viwanja. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...