Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii

BARAZA la Vyama vya Hiari na Maendeleo ya Jamii (Tacosode) limesema wananchi wamekuwa na uelewa kuhamasisha bajeti kuwa na kipaumbele kwa changamoto zinazowakabili.

Hayo ameyasema leo Meneja wa Miradi wa Tacosode, Koga Mihama wakati akizungumza waandishi wa habari juu wananchi kuwa na uelewa kuweka umuhimu bajeti katika halmashauri kutatua changamoto zinazowakabili.

Koga amesema kuwa uelewa huo umetokana na elimu waliopata katika mradi wa uhamasishaji wananchi kushiriki katika masuala ya afya katika kuangalia vipaumbele vya bajeti uliokuwa ukitekelezwa katika Mikoa ya Iringa pamoja na Dodoma.

Amesema kuwa wananchi mradi huo katika utekezwaji wake katika Halmashauri ya Iringa pamoja na Kongwa mkoani Dodoma wananchi wamekuwa na mwamko katika masuala ya afya ushiriki kwa kuchangia katika huduma za afya.

Koga amesema kuwa mradi huo ni wa miaka minne lakini umekuwa na matokeo katika wilaya ambazo umetekelezwa kwa wananchi kuwa na mwamko katika masuala ya huduma za afya kwa kuchangia hata nguvu zao pale panapobidi.

Aidha amesema kuwa mradi huo ukiisha wanaweza kufanya katika sekta zingine ili kuwa maendeleo ya katika masuala mbalimbali kutatuliwa.

Meneja wa Miradi wa Tacosode, Koga Mihama akizungumza na waandishi wa habari juu ya baraza hilo linavyofanya kazi katika mradi wa afya, leo jijini Dar es Salaam, Kulia ni Afisa Habari,Said Juma na Kushoto ni Afisa mradi wa Tacosode, Nobelrich Ekonea

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...