Afisa mwandamizi wa kilimo wa Burka Coffee Estates mkoani Arusha Bw. James Odhiambo (wa pili kushoto) akielezea jambo kwa mkurungezi wa kampuni ya Yara Tanzania Bw. Alexandre Macedo (kulia) walipotembelea shamba hilo pamoja na wataalamu wengine kutoka kwenye kampuni. 
Bw. Alexandre alisema moja ya vitu vikuu Yara Tanzania Ltd inajikita ni pamoja kuwapiga msasa wataalamu wa kampuni hiyo mara kwa mara ili waongeze ujuzi kwenye sekta hiyo na kuwasaidia wakulima kwa haraka wanapokutana na changamoto za kilimo upande wa mbolea.                    
"Wataalamu wetu wanao uwezo mkubwa wa kutambua ukosefu wa virutubisho kwenye mmea ila kama kampuni huandaa mafunzo kama haya ili kuwaongezea ujuzi wa kutambua na kutatua changamoto za mbolea wanazopata wakulima. Yara inatengeneza mipangilio maalumu ya lishe linganifu ya mimea baada ya tafiti  ya miaka mitatu. 
"Mfano mpangilio wa lishe ya zao la kahawa upo tayari na wakulima wanapewa semina mbalimbali kuhusu lishe hiyo kwani tafiti za udongo na virutubisho vinavyohitajika kwenye zao hilo ili liwe bora na mavuno yaongezeke ulishafanyika. 
"Ila kuna changamoto zingine hujitoteza ambazo wataalamu wetu hukumbushwa jinsi ya kuzitatua kupitia mafunzo kama haya ya mara kwa mara" Asema Bw. Alexandre
Picha ya zao freshi la kahawa iliyotapa virutubisho muhimu kupitia mbolea maalumu za zao hilo kutoka Yara Tanzania Ltd.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...