Kufuatia kukamilika kwa mchakato wa kufungua ubalozi wa Tanzania jijini Tel Aviv nchini Israel, na balozi mteule kuwasili kituoni, jana Alhamis tarehe 15 June 2017 Balozi wa Tanzania nchini humo, Mhe. Job Masima amewasilisha Hati za utambulisho kwa Mhe. Reuven Rivlin, Rais wa Taifa la Israel jijini Jerusalem.
Katika sherehe hiyo, Rais Rivlin alimshukuru Mhe. Dr John Pombe Joseph Magufuli, kwa kumteua balozi mkazi wa kwanza ubalozi nchini Israel . Ampongeza pia kwa hatua mbali mbali anazozichukua katika kukukuza uchumi na kusifia serikali yake kwa kudumisha hali ya utulivu na amani nchini Tanzania. Kwamba anaiona nchi ya Tanzania ikiwa yenye maendeleo makubwa mbeleni chini ya uongozi wake. Kwa upande wake, pamoja na mambo mengine, balozi aliwasilisha salamu maalimu za Rais Magufuli kwa Rais Ruvlin, serikali na wananchi wa Israel na kuahidi kudumisha mahusiani yaliyopo na yenye historia kubwa. Ubalozi wa Tanzania umepewa usajili wa kibalozi namba 88.
Balozi wa Tanzania nchini Israel Mhe. Masima akipokewa kwa nyimbo za taifa baada ya kuwasili kwenye Ikulu ya nchi hiyo mjini Jerusalem kabla ya kuwasilisha hati zake za utambulisho kwa Rais wa taifa hilo Mhe. Reuven Rivlin
Balozi wa Tanzania nchini Israel Mhe. Masima akijitambulisha kwa Rais wa taifa hilo Mhe. Reuven Rivlin kabla ya kuwasilisha hati zake za utambulisho
Balozi wa Tanzania nchini Israel Mhe. Masima akiwasilisha hati za utambulisho kwa Rais wa Taifa la Israel Mhe. Reuven Rivlin Ikulu ya nchi hiyo mjini Jerusalem
Akiwa amevaa baragashia ya kitamaduni ya Kiyahudi maarufu kama "Kippah" Balozi wa Tanzania nchini Israel Mhe. Job Masima akiwasilisha salamu za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na kusoma salamu maalumu za mwanzo wa urafiki mpya wa ushirikiano wa karibu kwa ki-Hebrew baada ya kuwasilisha hati za utambulisho kwa Rais wa Taifa la Israel Mhe. Reuven Rivlin Ikulu ya nchi hiyo mjini Jerusalem. Kwa picha zaidi BOFYA HAPA
Kwa taarifa zaidi za hafla hiyo BOFYA HAPA
Kwa taarifa zaidi za hafla hiyo BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...