Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akisalimiana na Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Msaada wa Kisheria {LSF} Tanzania Bwana Kees hapo Zanzibar Beach Resort Mazizini.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif akibonyeza kitufe cha Kompyuta kuashiria kuzindua rasmi Ofisi ya Taasisi ya Msaada wa Kisheria Zanzibar { LSF} hapo Hoteli ya Zanzibar Beach Resort Mazizini. Kulia ya Balozi Seif ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa LSF Jaji Jouquine De Mello na kushoto ya Balozi Seif ni Jaji Mkuu wa Zanzibar Mh. Omar Othman Makungu.
Balozi Seif akiagana Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Msaada wa Kisheria Tanzania {LSF} Jaji Jouquine De Mello baada ya kuizindua rasmi Ofisi ya Taasisi hiyo itakayokuwa mastakimu yake kwenye Jengo la ZSTC Kinazini Mjini Zanzibar. Picha na – OPMR – ZNZ.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...