Balozi wa Tanzania Nchini Burundi Mheshimiwa Rajabu Hassan Gamaha anayeangalia camera akizungumza na baadhi ya wajumbe wanaoshiriki Mkutano wa 8 wa Afrika Mashariki wa Sekta ya Petroli kutoka Wizara ya Nishati na Madini na Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ambao walifika katika Ofisi ya Ubalozi wa Tanzania jijini Bujumbura, Burundi leo kwa mazungumzo yaliyolenga kuimarisha uhusiano mwema ulipo baina ya Burundi na Tanzania. Ujumbe huo uliongozwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Dkt. Mhandisi Juliana L. Pallangyo aliyevaa suti nyeupe.

Mkurugenzi Mkuu wa EWURA Bwana Felix Ngamlagosi akisisitiza jambo wakati akizungumza na Balozi Rajabu juu ya uhusiano wa Taasisi ya EWURA na Taasisi mpya iliyoanzishwa Nchini Burundi  yenye jukumu la Kudhibiti Nishati ya Mafuta na Maji, pembeni yake ni Mkurugenzi Msaidizi Miundombinu ya Kiuchumi katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhandisi Abdillah Mataka.
Balozi Rajabu na Maafisa kutoka Wizara ya Nishati na Madini na Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki katika Mazungumzo hayo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...