Na.Vero Ignatus, Arusha.
Baraza la Wazee Jijini Arusha
wamemuomba Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe
Magufuli kuwaangalia wazee ambao walikuwa Jumuiya ya Afrika
Mashariki awalipe stahiki zao kwani wameifanyia nchi hii mambo
mazuri bali manufaa wameyakosa baada ya kuvunjika Jumuiya
hiyo.
Akizungumza na waandishi wa habari kwa niaba ya
wazee hao mwenyekiti wa Baraza hilo Mathius
Kichao amesema kuwa hadi sasa kuna wazee ambao
hawajalipwa stahiki zao jambo ambalo siyo zuri hata kidogo kwani wazee
hao wananung'unika
"Kuna
muda wazee hawa waliandamana wakenda Dar es salaam ,wakalala
barabarani,lakini viongozi wawakati ule hawakuona umuhimu kuwa kilio cha
wazee ni hatari sana wakawafukuzwa,nitamke kuwa hadi sasa kuna wazee wa
jumuiya ya Afrika Mashariki hawajalipwa chochote kile, niikumbushe
Serikali wale
wazee wanalaani ,naomba hii laana
isitokee,Mhe,Magufuli awalipe stahiki zao kwani wameifanyia nchi hii
vizuri zaidi "alisema Mwenyekiti huyo
Aidha wazee hao katika jiji la Arusha wameiomba serikali ya awamu ya tano ipeleke mswada wa wazee katika Bunge la Jamhuri ya Muungano na upitishwe ili Wazee nchini Tanzania waweze kunufaika na matunda ya nchi yao kwani wao ni chombo cha harakati hivyo Taifa likiwasahau wazee hakuna maendeleo kwasababu wazee huwa wanafahamu mambo mengi ya kihistotia ya Nchi pamoja na mila nzuri na desturi.
"Tunawaomba viongozi mbalimbali wa Taifa hili
wanapotembelea mkoa wa Arusha watenge muda wao ili waweze kuonana na
wazee tutawashauri kwa yale tunayoyafahamu kwaajili ya manufaa ya nchi
yetu na watoto pamoja na wajukuu zetu.
Mwenyekiti wa Baraza la wazee mkoa wa Arusha Mathius Kichao aliyeshika karatasi mkononi,akiwa anazungumza na waandishi wa habari hivi katibuni Jijini hapo.Picha na Vero Ignatus Blog.
Katibu wa wazee wa Baraza la wazee Jijini Arusha Kassim Seremuka akizungumza jinsi ambavyo wazee hao wamenifaika na vitambulisho vya bima ya afya .Picha na Vero Ignatus Blog.
Baadhi ya viongozi na wajumbe wa Baraza la wazee katika mkoa wa Arusha wakiwa katika picha ya pamoja .Picha na Vero Ignatus Blog.
Katibu wa Baraza la wazee Kassim Seremuka Jiji la Arusha akionyesha Kadi ya matibabu wanazotumia wazee wakienda kutibi wa Hospitalini.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...