Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH)  leo imemtia mbaroni kijana mmoja aliyekuwa akijifanya daktari.  Mtuhumiwa alikuwa akijitambulisha kwa wagonjwa kwamba anaitwa Dk Abdallah Juma na akijifanya kutoa huduma katika Maabara Kuu. 
Uongozi wa hospitali hiyo umesema kuwa kijana huyo ni daktari feki na si daktari kama alivyokuwa akijitambulisha na kwamba amekamatwa baada ya kuwekewa mtego na askari wa hospitali hiyo. Uongozi wa hospitali hiyo umesema kuwa walinzi walikuwa wakimtilia shaka na kuanza kumfuatilia hadi walipofanikiwa kumkamata. 
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Huduma kwa Wateja wa Hospitali hiyo, Aminiel Aligaesha amesema hospitali imeweka mikakati mbalimbali ya kupambana na wahalifu wakiwamo watu wanaojiita ni madaktari kama huyo ambaye amekamatwa leo.
 Kulia ni daktari feki ambaye amekuwa akijitambulisha kwamba ni Dkt, Abdallah Juma ambaye amekuwa akifanya kazi katika Maabara Kuu, katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) akiwa chini ya ulinzi baada ya kukamatwa na mmoja wa askari wa Muhimbili (kushoto).
Daktari feki huyo ambaye amekuwa akijitambulisha kwamba ni Dkt. Abdallah Juma akiwa chini ya ulinzi

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...