Benki ya CRDB ndio benki yenye huduma bora Tanzania kuliko benki nyingine yoyote, imeendeleo kuonyesha kuwajali Watanzania ambapo Menejmenti na Wafanyakazi wa CRDB Bank Tawi la Azikiwe Premier, la jijini Dar es Salaam, wameadhimisha Siku ya Mtoto wa Afrika, kwa kuwakumbuka watoto wanaoishi katika mazingira magumu, kwa kuwatembelea watoto wanaotunzwa katika kituo cha Jeshi la Wokovu kwa kuwapelekea zawadi mbalimbali za mahitaji muhimu, na kuwadhamini baadhi yao kwa kuwafungulia akaunti, kuwachangia, kugharimia elimu zao, na kugharimia mahitaji yao.

CRDB Azikiwe Premier Photo 8.JPG 
Wafanyakazi wa CRDB BANK, tawi la Azikiwe Premier, wakikabidhi zawadi mbalimbali kwa watoto wanaotunzwa katika kituo cha watoto wanaoishi katika mazingira magumu cha Jeshi la Wokovu, Kurasini jijini Dar es Salaam, wakati wa maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika ilioadhimishwa na benki hiyo kwa wiki nzima sasa.
CRDB Azikiwe Premier Photo 7.JPG 
Mfanyakazi wa CRDB BANK, tawi la Azikiwe Premier, akikabidhi zawadi mbalimbali kwa watoto wanaotunzwa katika kituo cha watoto wanaoishi katika mazingira magumu cha Jeshi la Wokovu, Kurasini jijini Dar es Salaam, wakati wa maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika ilioadhimishwa na benki hiyo kwa wiki nzima sasa.
CRDB Azikiwe Premier Photo 17.JPG 
Mkurugenzi na wafanyakazi wa CRDB Bank, Tawi la Azikiwe Premier, kwenye picha ya pamoja na mtoto Mariam Stephen Jackson, aliyekuwa akiishi katika mazingira magumu. Marriam pia amefunguliwa akauti maalum ya watoto ya benki hiyo iitwayo Junior Jumbo,ambayo wafanyakazi wa Tawi hilo la Azikiwe Premier, wananchangia kugharimia elimu yake. Sherehe hiyo imefanyika wakati wa maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Africa ilioadhimishwa na benki hiyo kwa wiki nzima sasa.
CRDB Azikiwe Premier Photo 19.JPG 
Mkurugenzi na wafanyakazi wa CRDB Bank, Tawi la Azikiwe Premier, wakiwa na keki ya mtoto Mariam Stephen Jackson, aliyekuwa akiishi katika mazingira magumu. Marriam pia amefunguliwa akauti maalum ya watoto ya benki hiyo iitwayo Junior Jumbo,ambayo wafanyakazi wa Tawi hilo la Azikiwe Premier, wananchangia kugharimia elimu yake. Sherehe hiyo imefanyika wakati wa maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Africa ilioadhimishwa na benki hiyo kwa wiki nzima sasa.
CRDB Azikiwe Premier Photo 5.JPG 

Mkurugenzi wa CRDB Bank, Tawi la Azikiwe Premier, Fabiola Musula, na wafanyakazi wa tawi hilo, na wateja, wakionyesha fedha walizomchangia mtoto Mariam Stephen Jackson, aliyekuwa akiishi katika mazingira magumu. Marriam pia amefunguliwa akauti maalum ya watoto ya benki hiyo iitwayo Junior Jumbo,ambayo wafanyakazi wa Tawi hilo la Azikiwe Premier, wananchangia kugharimia elimu yake. Sherehe hiyo imefanyika wakati wa maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Africa ilioadhimishwa na benki hiyo kwa wiki nzima sasa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...