Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

BENKI ya CRDB imeadhimisha siku ya  Mtoto wa Afrika kwa kuwapatia zawadi watoto mbalimbali ambao wazazi wao waliwafungulia akaunti za Junior Jumbo huku wakiwa wamewekewa fedha mara kwa mara.

Akitoa zawadi hizo, Mkurugenzi wa Tawi la Benki ya CRDB Azikiwe  Nomina Msoka amesema kuwa watoto hao waliopatiwa zawadi ni kutokana na wazazi wao kuwawekea fedha mara kwa mara na hata akiba za akaunti zao zina kiasi kikubwa cha fedha.

Nomina amesema kuwa, wazazi wanatakiwa kuwafungulia na kuwawekea watoto wao fedha mara kwa mara iili kuwandaa na maisha ya baadae ikiwemo katika kulipia ada za masomo yao na pia upo taratibu wa wazazi kuwaekea hela kupitia akaunti zao..

Amesema mbali na hilo, CRDB wameweza kuandaa michezo mbalimbali ya watoto kwa ajili ya kujumuika pamoja na wenzao na kufahamiana zaidi.
Mkurugenzi wa Tawi la Benki ya CRDB Azikiwe  Nomina Msoka akiwa amembeba mtoto Kinora Brown na kumkabidhi zawadi yake ya begi la Junoir Jumbo Akaunti  kwa mama yake wakati wa maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika yanayoadhimishwa Juni 16 kila mwaka. 
 Mkurugenzi wa Tawi la Benki ya CRDB Azikiwe Nomina Msoka akimkabidhi zawadi ya begi la Junoir Jumbo Akaunti  mtoto Orley Mwanyika wakati wa maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika yanayoadhimishwa Juni 16 kila mwaka.
 Mkurugenzi wa Tawi la Benki ya CRDB Azikiwe Nomina Msoka akimkabidhi zawadi ya begi la Junoir Jumbo Akaunti  mtoto Tonia Naivasha  wakati wa maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika yanayoadhimishwa Juni 16 kila mwaka.
  Mkurugenzi wa Tawi la Benki ya CRDB Azikiwe Nomina Msoka akimkabidhi zawadi ya begi la Junoir Jumbo Akaunti  mtoto Rashidi Jumbe wakati wa maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika yanayoadhimishwa Juni 16 kila mwaka.
  Mkurugenzi wa Tawi la Benki ya CRDB Azikiwe Nomina Msoka  akiwa katika picha ya pamoja na watoto aliowakabidhi zawadi za mebegi ya Junior Jumbo Akaunti  wakati wa maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika yanayoadhimishwa Juni 16 kila mwaka.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...