Dawasco inawatangazia wateja wake wote wakazi wa Jiji la Dar es Salaam, pamoja na
Mji wa Kibaha na Bagamoyo mkoani Pwani wenye madeni ya bili za Maji kwa kipindi cha
zaidi ya Mwezi mmoja kuwa, wanatakiwa kulipa madeni yao kabla ya tarehe
11.06.2017, kinyume na hapo Dawasco inakusudia kuwafikisha Mahakamani wateja
wote wanaodaiwa kipindi hicho cha zaidi ya mwezi mmoja.
Taarifa hii inawahusu wateja wote wenye madeni pamoja na wale watakaoshindwa
kulipa madeni yao ndani ya muda uliotajwa.
Mteja atakayeshindwa kulipa deni lake ndani ya muda tajwa atalazimika kulipia bili
yake, pamoja na gharama zote za kuendesha kesi kwa wale watakaofikia hatua ya
kufunguliwa mashtaka na faini.
Kumbuka Dawasco haipokei Malipo taslimu (Mkononi), malipo yote yafanyike kupitia
huduma za Kibenki, mawakala wa Selcom na Maxcom, pamoja na mitandao yote ya
simu ambayo imeidhinishwa.
Kwa maelezo zaidi wasiliana nasi kupitia kituo chetu cha huduma kwa wateja kwa
namba 0800110064 (BURE)
IMETOLEWA NA MKURUGENZI MKUU
DAWASCO
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...