Dawasco inawatangazia wateja wake wote wakazi wa Jiji la Dar es Salaam, pamoja na Mji wa Kibaha na Bagamoyo mkoani Pwani wenye madeni ya bili za Maji kwa kipindi cha zaidi ya Mwezi mmoja kuwa, wanatakiwa kulipa madeni yao kabla ya tarehe 11.06.2017, kinyume na hapo Dawasco inakusudia kuwafikisha Mahakamani wateja wote wanaodaiwa kipindi hicho cha zaidi ya mwezi mmoja.

Taarifa hii inawahusu wateja wote wenye madeni pamoja na wale watakaoshindwa kulipa madeni yao ndani ya muda uliotajwa.

Mteja atakayeshindwa kulipa deni lake ndani ya muda tajwa atalazimika kulipia bili yake, pamoja na gharama zote za kuendesha kesi kwa wale watakaofikia hatua ya kufunguliwa mashtaka na faini.

Kumbuka Dawasco haipokei Malipo taslimu (Mkononi), malipo yote yafanyike kupitia huduma za Kibenki, mawakala wa Selcom na Maxcom, pamoja na mitandao yote ya simu ambayo imeidhinishwa.

Kwa maelezo zaidi wasiliana nasi kupitia kituo chetu cha huduma kwa wateja kwa namba 0800110064 (BURE)

IMETOLEWA NA MKURUGENZI MKUU
DAWASCO

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...