Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii 

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Ally Hapi ameiagiza Mamlaka ya mapato nchini TRA ngazi ya Wilaya ya Kinondoni kubadilisha mfumo wa ukusanyaji wa kodi ili kuongeza mapato ya serikali kutoka Bilioni 40 na kuendelea.

Hapi amesema hayo katika ufunguzi wa mkutano wa Baraza la Wafanyabiashara la Wilaya ya Kinondoni  katika hoteli ya Traventine Magomeni, amesema kuwa serikali ni lazima ikusanye kodi ambayo inatokana na wafanyabiashara.

Hapi amesema  kuwa  kufikia malengo ya zaidi ya  ukusanyaji wa sh. bilioni  40  kwa kuwaingiza katika mfumo wafanyabiashara ndogo ndogo (Machinga) kwa kuwa na vitambulisho maalum ili waweze kulipa kodi .

Amesema  kuwa kuwaingiza machinga katika mfumo  ndio utakuwa urasimishaji wa machinga hao kwa kuweza kukopesheka katika taasisi za fedha ikiwa ni pamoja kwa TRA  kuweka vituo vya forodha katika Bandari Bubu za Mbweni ili kudhibiti mizigo inayoingia kinyemela  kutokea visiwa Zanzibar.

Mkuu wa Wilaya, Hapi Amesema kuwa kumekuwa na tatizo la uwepo wa leseni feki za biashara ambazo zinatolewa na watu feki nje ya ofisi za TRA na Manispaa ili waweze kukwepa kodi na kutafuta rekodi mpya ya wafanyabiashara ambao wamekuwa wakibuka kila siku katika Wilaya hiyo ambao wanastahili kulipa kodi kwa kuanza kupewa elimu.
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Ally Hapi akizungumza wakati wa uzinduzi wa Baraza la Wafanyabiashara Wilaya ya Kinondoni katika mkutano uliofanyika katika Ukumbi wa Traventine Magomeni.
Afisa Biashara wa Manispaa wa Manispaa ya Kinondoni, Mohamed Nyasama akizungumza juu ya hali ya biashara  katika Manispaa hiyo .
Sehemu Wajumbe wa Baraza la Wafanyabiashara la Wilaya ya Kinondoni katika mkutano uliofanyika katika Hotel ya Traventine Magomeni leo jijini Dar es Salaam

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...