Kampuni
ya mawasiliano ya simu ya Halotel, imezindua kampeni mpya ya Switch to
Halotel, yenye lengo la kuwahamasisha Watanzania kujiunga na Mtandao huo
sambamba na kuzindua utaratibu wa wafanyakazi wa kampuni hiyo
kuwatembelea wateja wa Mtandao huo katika maeneo yote nchi nzima mjini
na vijijini.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa Kampeni hiyo iliyofanyika katika soko la Makumbusho lililoko Kinondoni Dar es Salaam, Naibu Mkurugenzi wa Kampuni hiyo Mr Nguyen Van Son, amesema tangu kuzinduliwa kwa huduma za kampuni hiyo, wamepata mapokezi mazuri kutoka kwa watanzania ambao hadi sasa zaidi ya wateja milioni tatu na laki tano, tayari wamejiunga na mtandao huo na wanafurahia huduma mbalimbali zinazotolewa na kampuni hiyo ya simu.
“Tunafarijika sana kwa namna ambavyo Watanzania wameendelea kutuunga mkono katika jitihada zetu za kuboresha huduma za mawasiliano kwa jamii hii, ni faraja kubwa kwetu kwamba katika kipindi hiki kifupi tumepata mafanikio makubwa na bado tunaendelea kupata wateja wanaojiunga na mtandao wetu siku hadi siku,” Jambo hili linatufanya tusilale tufikilie ni namna gani tunapaswa kuendelea kukizi mahitaji yao.
“Kuzinduliwa kwa kampeni hii itakuwa ni sehemu ya sisi kusogea karibu na wateja wetu, kuwahudumia pamoja na kuwasikiliza ni nini wanahitaji kutoka kwetu,” Tunaamini kabisa kwamba kuwa karibu na wateja wetu tutajenga mtandao bora kabisa utakao kuwa na huduma zinazolenga maisha halisi ya Watanzania.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa Kampeni hiyo iliyofanyika katika soko la Makumbusho lililoko Kinondoni Dar es Salaam, Naibu Mkurugenzi wa Kampuni hiyo Mr Nguyen Van Son, amesema tangu kuzinduliwa kwa huduma za kampuni hiyo, wamepata mapokezi mazuri kutoka kwa watanzania ambao hadi sasa zaidi ya wateja milioni tatu na laki tano, tayari wamejiunga na mtandao huo na wanafurahia huduma mbalimbali zinazotolewa na kampuni hiyo ya simu.
“Tunafarijika sana kwa namna ambavyo Watanzania wameendelea kutuunga mkono katika jitihada zetu za kuboresha huduma za mawasiliano kwa jamii hii, ni faraja kubwa kwetu kwamba katika kipindi hiki kifupi tumepata mafanikio makubwa na bado tunaendelea kupata wateja wanaojiunga na mtandao wetu siku hadi siku,” Jambo hili linatufanya tusilale tufikilie ni namna gani tunapaswa kuendelea kukizi mahitaji yao.
“Kuzinduliwa kwa kampeni hii itakuwa ni sehemu ya sisi kusogea karibu na wateja wetu, kuwahudumia pamoja na kuwasikiliza ni nini wanahitaji kutoka kwetu,” Tunaamini kabisa kwamba kuwa karibu na wateja wetu tutajenga mtandao bora kabisa utakao kuwa na huduma zinazolenga maisha halisi ya Watanzania.
Naibu
Mkurugenzi wa Halotel, Nguyen Van Son akiweka Laini ya simu ya Halotel
kwa mteja mpya wa Mtandao huo, Simon Mkumbo, ambae amejiunga na Mtandao
huo wakati wa uzinduzi wa kampeni ya “Switch to Halotel” yenye lengo la
kuwahamasisha Watanzania kujiunga na Mtandao huo, Kampeni hiyo pia
itahusisha wafanyakazi wa Mtandao huo kutembelea maeneo mbalimbali na
kutoa huduma kwa wateja katika maeneo yao.
Meneja
Mawasiliano wa Halotel, Hindu Kanyamala, kwa pamoja na Naibu Mkurugenzi
wa Kampuni hiyo, Nguyen Van Son, wakitoa maelezo juu ya huduma za
mtandao huo kwa wafanya biashara wa Matunda wa soko la Makumbuso, Wakati
wa uzinduzi wa huduma ya” Switch to Halotel” yenye lengo la kuhamasisha
Watanzania kujiunga na Mtandao huo, Pamoja na wafanya kazi wa Mtandao
huo kutembelea maeneo mbalimbali kutoa huduma kwa wateja. Pamoja nao
katika picha ni Mkurugenzi wa Tawi la Dar es Salaam Vu Huy Thiem.
Meneja
Mawasiliano wa Halotel, Hindu Kanyamala, kwa pamoja na Naibu Mkurugenzi
wa Kampuni hiyo, Nguyen Van Son, wakitoa maelezo juu ya huduma za
mtandao huo kwa wafanya biashara wa Matunda wa soko la Makumbuso, Wakati
wa uzinduzi wa huduma ya” Switch to Halotel” yenye lengo la kuhamasisha
Watanzania kujiunga na Mtandao huo, Pamoja na wafanya kazi wa Mtandao
huo kutembelea maeneo mbalimbali kutoa huduma kwa wateja. Pamoja nao
katika picha ni Mkurugenzi wa Tawi la Dar es Salaam Vu Huy Thiem.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...