Afisa wa Kitengo cha Rasilimali watu Zantel, Maryam Khatri (kushoto) akitoa huduma ya chakula kwa Mkurugenzi Mkuu wa Zantel Benoit Janin (kulia) katika tafrija ya futari iliyofanyika jana jijini Dar es Salaam. Tafrija hiyo ilikuwa ni mahususi kwa ajili ya wafanyakazi na wadau wa kampuni hiyo.
Baadhi ya wafanyakazi wa Zantel wakijumuika kupata futari katika tafrija iliyoandaliwa na Kampuni hiyo katika kipindi hiki cha mfungo Mtukufu wa Ramadhani ambayo ilifanyika jana jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa Zantel, Benoit Janin akizungumza wakati wa tafrija ya futari maalumu iliyoandaliwa na Kampuni hiyo kwa ajili ya wafanyakazi na wadau mbalimbali katika kipindi hiki cha mfungo Mtukufu wa Ramadhani. Tafrija hiyo ilifanyika jana jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Kitengo cha Rasilimali Watu Zantel Joanitha Mrengo akizungumza wakati wa tafrija ya futari maalumu iliyoandaliwa na Kampuni hiyo kwa ajili ya wafanyakazi na wadau mbalimbali katika kipindi hiki cha mfungo Mtukufu wa Ramadhani. Tafrija hiyo ilifanyika jana jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa Zantel, Benoit Janin (wa kwanza kushoto) akifurahia jambo na baadhi ya viongozi wa Kampuni hiyo wakati wa tafrija ya futari iliyoandaliwa na Zantel kwa ajili ya wafanyakazi na wadau mbalimbali katika kipindi hiki cha mfungo Mtukufu wa Ramadhani. Tafrija hiyo ilifanyika jana jijini Dar es Salaam. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...