Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala , Omary Kumbilamoto akikabidhi mchango wake wa shilingi laki tatu katika harambee ya kuchangia Madrassa ya Muumini Islamiya iIliyopo kiwalani Dar es Salaam
Meya wa jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita akikabidhi mchango wake kwa Katibu mkuu wa Chama cha Wananchi CUF, Maalim Seif Sharif Hamad kwa ajili ya Muumini islamiya.
Katibu mkuu wa Chama cha Wananchi CUF, Maalim Seif Sharif Hamad akiongoza harambee ya uchangiaji wa Madrasa Kiwalani Temeke jijini Dar es Salaam ambapo aliwezesha kupatika kwafedha zaidi ya Milioni 7 kwa ajili ya ununuzi wa kiwanja kipya cha Madrasa hiyo
Meya wa jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita akizungumza wakati alipokuwakitoa ahadi yake ya Milioni moja kwa ajili ya Madrasa hiyo na aliweza kuwasilisha shilingi laki tano papo hapo na kuongeza ahadi ya bati 70 na mifuko 50 ya Saruji.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...