Serikali ya Tanzania inafanya maboresho ya Mfumo wa Usajili uliopo na kuanzisha mfumo utakaofanya kazi vizuri usajili wa matukio muhimu ya binadamu na takwimu nchini unaofanywa na Wakala wa  Usajili, Ufilisi na Udhamini - RITA 
Waziri wa Katiba na  Sheria Prof.  Palamagamba  Kabudi  amesema hayo mjini Dodoma wakati akifungua mkutano wa wadau wanaojadili mfumo huo. Amesema maboresho ya mfumo huo yanatekelezwa kupitia Mkakati wa Kitaifa wa usajili wa Matukio muhimu ya binadamu na takwimu (Civil Registration and Vital STATISTICS-CVRS. 
Prof Kabudi amesema Mfumo huo unalenga kutatua changamoto mbalimbali ambazo zimefanya hali ya usajili wa Matukio muhimu ya binadamu kutokuwa ya kuridhisha nchini. Ameongeza kuwa ana imani kuwa utekelezaji wa mkakati huo itakuwa njia sahihi itakayowezesha kumuona kila mwananchi katika picha ya taifa.
Mkutano huo wa wadau wa usajili wa Matukio muhimu ya mwanadamu nchini umeandaliwa na RITA
Waziri Prof. Kabudi akipata picha na washiriki baada ya kufungua mkutano wa wadau wanaojadili mfumo huo. Amesema maboresho ya mfumo huo yanatekelezwa kupitia Mkakati wa Kitaifa wa usajili wa Matukio muhimu ya binadamu na takwimu (Civil Registration and Vital STATISTICS-CVRS. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...