Na Mwandishi Wetu 

Mwanasiasa mkongwe nchini Augustine Lyatonga Mrema amesema Rais John Pombe Magufuli ameweka historia ya mapambano ya uchumi nchini kutokana na namna ambavyo analishughulikia suala la madini.

Bwana Mrema amesema kuwa kitendo cha Mwenyekiti wa Kampuni ya Barrick Gold Cooperation Profesa John Thornton kusafiri usiku kucha kuja kuonana na Rais Magufuli na kukubali kuilipa Tanzania fedha zote ilizokoseshwa na Kampuni Acacia ni kielelezo kuwa sio tu kuwa ujumbe wake umefika lakini zaidi inadhihirisha kuwa madai yake dhidi ya kampuni hiyo ya uchimbaji madini ni ya msingi.

“Ni kiongozi gani barani Afrika aliyethubutu kuishutumu kampuni ya nje kama alivyofanya Rais Magufuli halafu viongozi wake wakasafiri kuonana na kiongozi huyo kutaka suluhu kama alivyofanya Mwenyekiti huyo wa Barrick kwa Tanzania?”alihoji Bwana Mrema.

Mwanasiasa huyo aliungana na wito wa Rais Magufuli wa kuwataka baadhi ya watu wanaowahusisha viongozi wastaafu na taarifa za Tume za Rais za kuchunguza Makinikia.

“Si vizuri na kwamba si sheria kwa mtu yeyote kuwatukana au kuwashambulia marais wastaafu kama ilivyo kwa Rais aliye maradakani na sheria inatoa dhabu kali kwa wanaofanya hivyo” alieleza bwana Mrema.

BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...