Mratibu wa Masoko wa Bayport Financial Services, Mercy Mgongolwa akimkabidhi kompyuta mbili Kaimu Mkurugenzi wa Mbulu, mkoani Manyara, Deogratias Kashasha.


Na Mwandishi Wetu, Mbulu
KWA miezi kadhaa sasa mvua imeendelea kunyesha katika mikoa mbalimbali ya Tanzania, hali inayoonyesha kukidhi kiu ya watu wengi waliokuwa wakiiomba inyeshe katika maeneo yao.

Hata hivyo, licha ya mvua hiyo kunyesha, lakini baadhi ya maeneo imekuwa na matokeo mabaya kutokana na kuezua nyumba, kuharibu miundo mbinu muhimu ikiwamo ya barabara.

Matokeo hayo yameibua changamoto mpya hususan za kufikika kwa urahisi katika maeneo hayo yanayoendelea kukumbwa na mvua kubwa. Mbali na mvua hiyo kunyesha, hata hivyo uwajibikaji unaendelea kufanyika kwa sekta na watu mbalimbali kuendelea na maisha yao ya kila siku ili wakuze uchumi.
Zoezi la kutoa msaada wa kompyuta lilivyokuwa linaendelea katika mikoa mbalimbali ya Tanzania.


Licha ya maeneo mengi kukumbwa na mvua, lakini Taasisi ya Kifedha ya Bayport Financial Services imeendelea na usambazaji wa kompyuta katika ofisi za serikali mikoani kama ilivyozindua utaratibu huo mwishoni mwa mwaka jana.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...