Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe (kulia) akizungumza na Balozi wa Uingereza nchini, Sarah Cooke ofisini kwake mjini Dodoma. Alimueleza balozi huyo kuwa Serikali imebaini na itakomesha ujanja unaofanywa na wafanyabiashara haramu wa kutakatisha fedha kwa kununua makundi makubwa ya mifugo na kuyachunga kwenye maeneo ya hifadhi nchini na baadae kuyauza kwa faida kwenye minada.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe (kulia) akifurahia jambo na Balozi wa Uingereza nchini, Sarah Cooke ofisini kwake mjini Dodoma.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe (kulia) akimkabidhi Balozi wa Uingereza nchini, Sarah Cooke majarida mbalimbali enye taarifa za vivutio vya Tanzania ofisini kwake mjini Dodoma. (Picha na Hamza Temba - WMU)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...