Na Nurdin Ndimbe

Kwa miaka ya hivi karibuni Mkoa wa Mtawara umekuwa na maendeleo makubwa ya Kichumi na ya Kisiasa. Kutokana na mabadiliko hayo maendeleo ya Mkoa wa Mtwara yameongeza ari na matumaini mapya ya maisha bora kwa wananchi wa Mkoa huo. 

Mtwara ya sasa ni yenye fursa lukuki kutokana na miradi mbalimbali ya maendeleo yaliyotokana na uchimbaji wa gesi asilia, maendeleo ya uboreshaji wa miundombinu na ongezeko na mapato katika zao la korosho.

Maendeleo haya yameikumba Sekta mbalimbali Mkoani humo ikiwemo ya Sekta ya Sheria hususani Mahakama. Mahakama ya Tanzania kanda ya Mtawara yenye watumishi 218 ilianza kutekeleza Mradi wa Mapambano dhidi Rushwa (Strengthening Tanzania Anti-Corruption Action ) kwa kifupi STACA Mwaka 2011/2012 chini ya ufadhili wa Uingereza kupitia Shirika lake la misaada la Kimataifa la DFID. 

Lengo kuu la mradi huu ilikuwa ni kuzuia na kupambana na rushwa mahala pa kazi, Katika Mkoa wa Mtwara mradi huu ulihusisha Wilaya zote tano za Tandahimba, Masasi, Newala, Mtwara na Nanyumbu. Mradi huu ulijikita katika ugawaji wa vitendea kazi kama kompyuta na ‘printer’ zake, mafaili ya kufungulia mashauri (case files), makabati ya kutunzia mafaili na kumbukumbu, pikipiki kwa watumishi wa Mahakama pamoja na baiskeli kwa ajili ya kusambazia ‘Summons.’
Baadhi ya pikipiki zilizotolewa chini ya Mradi wa STACA, pikipiki hizi na baadhi ya vifaa vingine tajwa ni miongoni mwa vitendea kazi vilivyotolewa kurahisisha utoaji huduma ya haki.
Muonekano wa picha ya bango lenye ujumbe wa kuzuia na kupambana na Vitendo vya Rushwa ikiwa imebandikwa katika jengo la Mahakama Kuu-Kanda ya Mtwara. Bango hili ni kati ya Mabango mengi ambayo yamebandikwa katika majengo ya Mahakama nchini lengo likiwa ni kuzuia rushwa na vitendo vitendo vyenye ukosefu wa maadili.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...