Wakuu wa Idara wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) wakijadili masuala mbalimbali walipotembelewa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa mamlaka hiyo, Bw. Ramadhan Maleta, katika mwanzo wa Wiki ya Utumishi wa Umma iliyoanza Juni 16-23 kwenye Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA).
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. Ramadhani Maleta akimsikiliza na Kaimu Mkurugenzi wa Kiwanja cha ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), Bw.Joseph Nyahende (kushoto), wakati wa kuadhimisha Wiki ya Utumishi wa Umma iliyoanza Juni 16 hadi 23. Wa pili kulia ni Kaimu Mkurugenzi Rasilimali Watu, Bw. Mohamed Ally na kushoto ni Mkurugenzi Viwanja vya Mikoa, Bw. Valentine Kadeha.
Mkuu wa Kitengo cha Usalama katika jengo la kuwasili na kuondokea abiria mashuhuri la VIP kwenye Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), Bw. Leonard Mbogoma (wapili kushoto)akimuelezea jambo Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. Ramadhan Maleta alipotembelea jengo hilo ikiwa ni maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma iliyoanza Juni 16-23.
Kaimu Mkurugenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), Bw. Joseph Nyahende akimfafanulia jambo Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. Ramadhan Maleta ikiwa ni siku ya kwanza ya Wiki ya Utumishi wa Umma iliyoanza Juni 16-23.
Ofisa Biashara wa JNIA, Bi. Herrieth Nyarusi (kushoto) akizungumza wakati Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. Ramadhan Maleta alipotembelea Idara ya Biashara kusikiliza kero na maoni kutoka kwa watumishi, ikiwa ni maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma. Kulia ni Meneja wa Fedha (JNIA), Bw.Shadrack Chilongani na katikati ni Bw. Godfrey Kanyama.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...