Umma unaarifiwa kuwa Serikali imefanya jitihada za kuwatafuta na hatimaye kuwapata ndugu wa marehemu Mzee Francis Maige Kanyasu (86) anayetajwa kuwa mmoja wa wachoraji wa nembo ya Taifa. Mzee Kanyasu alifariki dunia usiku wa tarehe 29 Mei, 2017 saa mbili na nusu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.
Mwili wa marehemu utaagwa rasmi katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kuanzia saa mbili na nusu asubuhi Jumamosi ya tarehe 3 Juni, 2017 na mara baada ya kuagwa mwili marehemu atasafirishwa na Serikali kwenda kijijini kwao Igokero, Wilaya ya Misungwi kwa ajili ya mazishi.
Taarifa zaidi kuhusu mazishi ya Mzee Kanyasu zitaendelea kutolewa kwa umma kadiri inapobidi.
Imetolewa na:
Bi. Sihaba S. Nkinga
KATIBU MKUU
Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto
(MAENDELEO YA JAMII)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...