Umma unaarifiwa kuwa Serikali imefanya jitihada za kuwatafuta na hatimaye kuwapata  ndugu wa marehemu Mzee Francis Maige Kanyasu (86) anayetajwa kuwa mmoja wa wachoraji wa nembo ya Taifa. Mzee Kanyasu alifariki dunia usiku wa tarehe 29 Mei, 2017 saa mbili na nusu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Mwili wa marehemu utaagwa rasmi katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kuanzia saa mbili na nusu asubuhi  Jumamosi ya tarehe 3 Juni, 2017 na mara baada ya kuagwa mwili marehemu atasafirishwa na Serikali kwenda kijijini kwao Igokero, Wilaya ya Misungwi kwa ajili ya mazishi.

Taarifa zaidi kuhusu mazishi ya Mzee Kanyasu zitaendelea kutolewa kwa umma kadiri inapobidi.

 Imetolewa na:

Bi. Sihaba S. Nkinga
KATIBU MKUU
Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto
(MAENDELEO YA JAMII)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...