Na. Catherine Sungura na Benson Mwaisaka,WAMJW- Kibaha

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Ummy Mwalimu amempongeza na kumshukuru Mhe.Dkt. John Pombe Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuongeza chachu katika mapambano dhidi ya malaria kwa kununua lita laki moja na kusambazwa kote nchini.

Ameyasema hayo wakati wa ugawaji wa Viuadudu vya kutokomeza mbu wa malaria kwa halmashauri kumi na moja zilizofika katika kiwanda cha kuzalisha Viuadudu hivyo kilichpo Mjini Kibaha

Aidha ,Waziri Ummy alisema anamshukuru Mhe. Rais kwa kumruhusu kuanza zoezi hilo kwa awamu ambapo kwa awamu ya kwanza Viuadudu hivyo vitagawiwa kwa Halmashuri 14 nchini ambazo zina viwango vikubwa vya maambukizi ya ugonjwa wa malaria,“hii ametupa nguvu na ari sisi tuliopo kwenye dhamana ya kusimamia sekta ya afya katika kupambana na Malaria.

Hata hivyo alisema kwa mujibu wa takwimu toka ofisi ya Takwimu nchini zinaonyesha kwamba kiwango cha maambukizi ya ugonjwa wa Malaria nchini ni asilimia 14 ambapo katika kila watoto walio chini ya miaka mitano kati ya watoto 100 watoto 14 wamekutwa na maambukizi ya Malaria

“Maelekezo yangu hasa kwa Waganga Wakuu wa Mikoa na Wilaya ni kuhakikisha dawa hii mnapulizia kuzingatia miongozo iliyotolewa na Wizara ya Afya,Muangalie ukubwa wa eneo la mazalia ya mbu,na kiasi kinachotakiwa kupulizia”.

Waziri Ummy amewataka wahakikishe wanapulizia Viuadudu hivyo angalau mara nne kwa mwezi kwa maana kila baada ya siku saba,hivyo ni lazima wanunue vifaa vya kupulizia dawa hii pamoja na kutoa mafunzo kwa watumishi watakaenda kufanya zoezi hilo.

Pamoja na hayo Waziri Ummy aliwataka ifikapo mwisho wa mwezi huu kila Mkurugenzi wa Halmshauri awe ampelekee mahitaji halisi ili kuona ni jinsi gani watatekeleza kazi hiyo “Lazima nipate mahitaji halisi toka Halmashauri kwa kuwa Mhe. Rais ameshatuonyesha njia na ametuelekeza badala ya kununua dawa pia tununue na viuadudu hivi”

Naye Mkurugenzi Msaidi toka Wizara ya Viwanda,Biashara na Uwekezaji Mhandisi Elli Pallangyo alisema leo hii Halmashauri kumi na moja sawa na Mikoa sita ndizo zilizofika katika uzinduzi huo wa ugawaji wa Viuaduddu kwa awamu ya kwanza,alizitaka Halmashauri hizo na mgawanyo wa lita kwenye mabano

Liwale(1,200), Tarime (384), Misungwi(1,296), Kasulu(540), Songea(816),Kakonko(660), Kisarawe(720), Kyerwa(1,080), Rufiji(5,088), Geita(2,100), Kilombero(1,140)
Matukio mbaljmbali zikionyesha matukio wakati wa ugawaji Viuadudu vya kutokomeza Mbu wa Malaria Mjini kibaha.Pichani ni Waziri Ummy Mwalimu akigawa Viuadudu hivyo kwa Halmashauri kumi na moja

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...