Watoto na vijana 50 kutoka mikoa ya Geita,Mwanza na Shinyanga wanaoshiriki katika kambi ya Ariel 'Ariel Camp 2017’  jijini Mwanza iliyoandaliwa na shirika la Ariel Glaser Pediatric Aids Healthcare Initiative (AGPAHI) linalojihusisha na mapambano dhidi ya Virusi vya Ukimwi (VVU) na Ukimwi, wametembelea makumbusho ya kabila la Kisukuma   ‘Sukuma Museum’ ya Bujora Kisesa Mwanza ili kujifunza tamaduni na mila za Kisukuma. 
Bango linaloonesha makumbusho ya Kisukuma ya Bujora Mwanza,pichani kushoto ndiye mwanzilishi wa makumbusho hayo David Clement Fumbuka aliyezaliwa mwaka 1922 na kufariki dunia mwaka 1986.
Mwongozaji wa wageni katika makumbusho ya Kisukuma Bujora ,Yasinta Salum akielezea historia ya makumbusho hayo kwa watoto na vijana kutoka mikoa ya Shinyanga,Geita na Mwanza walioshiriki katika Kambi ya Ariel jijini Mwanza.
Yasinta akiendelea kutoa historia ya Makumbusho ya Bujora.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...