Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel kwa kushirikiana na Dar Teknohama Business Incubator (DTBi) leo imezundua maabara ya kompyuta ilijulikanayo kama  “Airtel Fursa Lab” katika shule ya msingi ya kijitonyama wilaya ya Kinondoni kwa lengo la kuwawezesha vijana kupata ujuzi katika masomo ya Tehama na kukuza ujuzi katika maswala ya kitechnologia
  
Maabara hiyo ya “Airtel Fursa Lab” itatoa mafunzo ya msingi ya kompyuta kwa hatua ya awali  na mafunzo ya hatua ya juu zaidi kwa  wanafunzi wa shule za msingi, sekondari, chuo kikuu na jamii nzima kwa ujumla. Walimu pia watapata mafunzo ya kompyuta yatakayowawezesha kutoa msaada kwa wanafunzi watakaotumia maabara hiyo

Akizindua maabara hiyo mgeni rasmi ambaye ni  Katibu Mkuu ofisi ya Waziri Mkuu, Prof. Faustin Kamuzora aliwapongeza Airtel na DTBi kwa kuweka nguvu pamoja  katika ushirikiano huu ambao utachochea mapinduzi kwa vijana wa kitanzania katika sekta ya habari namawasiliano (ICT).  Hii itasaidi kujenga jamii yenye msukumo wa kutafuta masuluhisho na kujiongezea wigo katika ujasiliamalia ambayo utasaidia kukuza uchumi wa viwanda kwa taifa”

Pia alitoa wito kwa wadau wengine kuunganisha nguvu katika ushirikiano kama huo ili kuleta maendeleo zaidi”

Akiongea katika uzinduzi huo pia, Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel, Beatrice Singano Mallya alisema “ wakati Tanzania imejipanga kufikia uchumi wa viwanda mahitaji ya wafanyakazi wenye ueledi katika teknologia wanahitajika sana ili kufikia malengo haya. Hivyo ni muhimu kujenga vijana wenye ujuzi  na ueledi wakiwa katika umri mdogo na hivyo tunajisikia fahari kuwa sehemu ya kutoa ujuzi na kukuza maendeleo ya watanzania katika Teknologia ya Tehama kupitia maabara ya Airtel Fursa  tunayozindua leo.

Maabara ya Airtel Fursa ni uthibitisho wa dhamira yetu ya kutumia teknologia ya mawasiliano ya simu pamoja na Tehama katika kustawisha biashara na kukuza ujuzi katika teknologia  na hivyo kuwa na nguvukazi yenye ueledi zaidi.  Natoa wito kwa vijana na jamii nzima kuchangamkia fursa hii na kuitumia maabara hii ya kompyuta ipasavyo. Aliongeza Mallya

  Katibu Mkuu ofisi ya Makamu wa Rais , Prof. Faustin Kamuzora (katikati) akiongea wakati wa uzinduzi wa maabara ya Kompyuta itakayojulikana kama“Airtel Fursa Lab” ili kufundisha watoto na vijana mafunzo ya TEHAMA chini ya usimamizi na ushirikiano kati ya Airtel na Dar Teknohama Bussiness Incubator (DTBI)  kulia ni Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel Bi, Beatrice Singano na Mkurugenzi Mkuu wa DTBI Eng. George Mulamula (kushoto). “Airtel Fursa Lab” imezinduliawa leo kwenye shule ya msingi ya kijitonyama iliyoko wilaya ya Kinondoni.
 Katibu Mkuu ofisi ya Makamu wa Rais , Prof. Faustin Kamuzora (wapili kulia) akikata utepe ili kuzinduzia  maabara ya Kompyuta ya “Airtel Fursa Lab” ili kufundisha watoto na vijana mafunzo ya TEHAMA chini ya usimamizi na ushirikiano kati ya Airtel na Dar Teknohama Bussiness Incubator (DTBI)  kulia ni Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel Bi, Beatrice Singano na Mkurugenzi na kushoto kwake ni Mkuu wa DTBI Eng. George Mulamula na Mwenyekiti wa kamisheni ya ICT Tanzania Maharage Chande na Mweyekiti wa Bodi ya Shule ya msingi Kijitonyama John Mutajwaha “Airtel Fursa Lab” imezinduliawa leo kwenye shule ya msingi ya kijitonyama iliyoko wilaya ya Kinondoni.
 kushoto ni Mwanafunzi wa shule ya msingi  Aghakan Serira Telerico akielezea jinsi alivyotengeneza program ya Robot  kwa Katibu Mkuu ofisi ya Makamu wa Rais , Prof. Faustin Kamuzora wakati alipozindua Maabara hiyo  kwenye shule ya msingi ya kijitonyama wilaya ya kinondoni, wanaoshudia ni Mkuu wa DTBI Eng. George Mulamula na Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel Bi, Beatrice Singano ambao ndio wasimamizi na wadhamini wa  Maabara hiyo. “Airtel Fursa Lab” imezinduliwa leo kwa lengo la kuwawezesha vijana kupata ujuzi katika masomo ya Tehama na kukuza ujuzi katika maswala ya kitechnolojia
Mwanafunzi wa shule ya msingi  Aghakan mzizima Brayan Basimaki (wakwanza kushoto) akielezea jinsi anavyotengeneza program zake za kompyuta  kwa Katibu Mkuu ofisi ya Makamu wa Rais , Prof. Faustin Kamuzora wakati alipozindua Maabara hiyo  kwenye shule ya msingi ya kijitonyama wilaya ya kinondoni, Maabara hiyo. “Airtel Fursa Lab” imezinduliwa leo kwa lengo la kuwawezesha vijana kupata ujuzi katika masomo ya Tehama na kukuza ujuzi katika maswala ya kitechnologia.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...