MSHINDI wa Sh Milioni 20 kutoka Bahati Nasibu ya Biko,
Leonard Bagumako, amesema ameyavulia kofia mamilioni ya Biko, baada ya
kukabidhiwa huku akiwa hakufahamu lolote kwamba yeye angeweza kuyatwaa.
Bagumako aliyasema hayo jana wakati anakabidhiwa fedha zake
jumla ya Sh Milioni 20, katika benki ya NMB, jijini Dar es Salaam, huku akiwa
kijana mwenye umri wa miaka 21 tu anayefanya shughuli za uuzaji wa duka
Kigamboni.
Akizungumzia fedha hizo, Bagumako alisema awali aliamini kuwa
mchezo wa Biko unahusu watu matajiri, lakini baada ya kukabidhiwa fedha hizo,
ameamini kila Mtanzania bila kuangalia wapi anaishi na uchumi wake anaweza
kuibuka kidedea kwa kupata ushindi.
“Biko nimewavulia kofia kwa sababu kumbe hata sisi mafukara
tunaweza kushinda zawadi mbalimbali za biko kuanzia Sh 5,000, 10,000, 20,000,
50,000, 100,000, 500,000 na Sh Milioni moja za papo kwa hapo, bila kusahau
ushindi mnono wa Sh Milioni 20 kama niliyoupata mimi,” Alisema.
Naye Mratibu wa Matukio na Mawasiliano wa Biko, Hassan
Melles, alisema baada ya kumkabidhi Bagumako fedha zake, wanashauku kubwa ya
kumkabidhi mtu mwingine Milioni 20 atakayetokana na droo ya 27 itakayofanyika
Jumapili, jijini Dar es Salaam.
“Bagumako ameshapata fedha zake na mwingine atapokea kutoka
droo kubwa ya Jumapili, ambapo Biko tunaamini yoyote anaweza kuibuka na ushindi
huo mnono kwa kucheza biko kwa mitandao ya simu Tigo Pesa, M-Pesa na Airtel
Money kwa kufanya miamala kuanzia Sh 1,000 na kuendelea ambapo namba yetu ya
kampuni ni 505050 na kumbukumbu ni 2456.
“Namna ya kucheza ni rahisi kwa sababu mshiriki atafanya
muamala kulingana na matakwa ya mtandao wake, huku kiasi cha Sh 1,000 kikiwa na
nafasi mbili, ushindi wa papo kwa hapo pamoja na kuingia kwenye droo kubwa ya
kuwania Sh Milioni 20 inayofanyika Jumapili na Jumatano,” Alisema.
Kwa kipindi cha miezi miwili ya Mei na Juni, tayari bahati
nasibu ya Biko, wameshatoa zaidi ya Sh Bilioni moja kwa washindi wa papo kwa
hapo na donge nono la Sh Milioni 20 linalotoka kila Jumatano na Jumapili.
Mratibu wa Matukio na Mawasiliano, Hassan Melles kulia akimkabidhi jumla ya Sh Milioni 20 mshindi wao wa droo ya 26 ya Biko, Leonard Bagumako wa pili kutoka kulia. Wengine pichani ni baba mlezi wa Bagumako, Gerlad Madaraka kushoto pamoja na mtumishi wa NMB, Tawi la Bank House, jijini Dar es Salaam.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...