CHAMA cha riadha Mkoa wa Singida kimeshauriwa kuangalia uwezekano wa kuzitafutia ufumbuzi baadhi ya changamoto zinazochangia idadi kubwa ya wanawake kutopenda na kisha kutoshiriki kabisa katika mchezo wa riadha.

Akitoa ushauri huo kwenye viwanja vya michezo vya shule ya msingi Tambukareli,wilayani Manyoni,Mkoani Singida,mmoja wa washiriki wa mashindano hayo,Hamida Nasoro alisisitiza kuwa kutokana na idadi kubwa ya wanawake kutohamasishwa kushiriki katika mashsindano hayo,ndiko kulikochangia mashindano ya mchezo huo wa riadha kuwa na idadi ndogo ya washirki.

“Mashindano haya tumeonekana wanawake wachache sana labda ni kwa ajili ya changamoto mbali mbali ikiwemo wanawake wengi kutopenda kujishirikisha katika mchezo wa riadha kunakotokana na ukuaji wao wa umri”alisisitiza Hamida.

Akizungumza na kituo hiki,Hamida hata hivyo hakusita pia kutoa tahadhari kwa wanawake wanaopenda kushiriki katika mchezo huo wa riadha wasijihusishe katika mahusiano ya kimapenzi kwani endapo wataendelea kufanya hivyo,ndoto zao za mafanikio katika mchezo huo zitapotea.
Hata hivyo Hamida alitumia fursa ya mashindano hayo kuwashauri wanawake wasiopenda kushiriki mchezo huo wajenge utamaduni wa kupenda kushiriki mchezo huo ili waweze kulitangaza soko la mchezo huo kwa wanawake.
Baadhi ya washiriki wa mashindano ya mchezo wa riadha wa Mkoa wa Singida walioshiriki mashindano hayo yaliyofanyika katika viwanja vya michezo vya shule ya msingi Tambukareli,wilayani hapa.
Mwanamke mwenye umri wa miaka 48,Zainabu Ramaddhani kutoka wilaya ya Ikungi akishiriki mbio za umbali wa kilomita 21 katika mashindano hayo na kufanikiwa kuchaguliwa kwenda kushiriki mashindano ya kimkoa.(Picha zote Na Jumbe Ismailly).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...