Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi amewapongeza wana kijiji cha Ghalunyangu kilichopo kata ya Makuro Wilayani Singida kwa uzalendo wa kujitolea nguvu kazi ya kuchimba mtaro wenye urefu wa mita 670 katika mradi wa maji kijijini hapo.
Dkt Nchimbi ametoa pongezi hizo mara baada ya kushuhudia mtaro huo utakaopitisha maji kutoka katika chanzo cha maji hadi katika tenki la ukubwa wa lita elfu 10 na kuelekea katika vituo vitatu vya kuchotea maji ikiwa ni jitihada za kufanikisha ukarabati wa mradi wa maji kijijini hapo.
Amesema “nguvu ya kuchimba mtaro huu haitaenda bure, tuna uhakika maji yatafika katika vituo hivyo vitatu kwa kuanzia ili kuwaepusha kuendelea kuchota maji katika bomba moja lililopo eneo la chanzo cha maji”.
Dkt Nchimbi ameongeza kuwa, “uzalendo huu usiishie kwenye kuchimba mtaro tu, nawaomba mtoe ushauri na mapendekezo ili ukarabati wa mradi huu uwe wa ufanisi mkubwa, na hata mkiona mambo yanaenda ndivyo sivyo toeni taarifa mapema, lakini nina imani na halmashauri ya Singida, itatekeleza kwa ufanisi mradi huu kwa manufaa yenu wana Ghalunyangu”.
Aidha amewataka wana kijiji hao kuwa walinzi wa miundo mbinu ya mradi huo pamoja na kutunza chanzo cha maji hasa kwa kuongeza eneo la hifadhi ya chanzo cha maji kutoka mita 60 mpaka mita 100 na kupanda miti ya kutosha katika chanzo hicho.

 Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi akizungumza na fundi anayejenga mnara wa kuweka tanki la maji la lita elfu 10 katika kijiji cha Ghalunyangu, Wilayani Singida.
 Mhandisi wa Maji Mkoa wa Singida Mhandisi Lydia Joseph (aliyeinama) akikagua mabomba yatakayotumika kupeleka maji kwenye vituo vitatu vya kuchotea maji katika kijiji cha Ghalunyangu, Wilayani Singida.
 Wanakijiji cha Ghalunyangu wakichota maji katika bomba pekee lililopo katika chanzo cha maji na maradi wa maji kijijini hapo. Fedha za malipo kwa matokeo zimeelekezwa kijijini hapo ili kujenga vituo vitatu vya kuchotea maji kwa kuanzia ikiwa vituo vingine vitajengwa hapo baadaye.
 Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi akizungumza na wana kijiji cha Ghalunyangu, Wilayani Singida waliokusanyika katika chanzo cha maji na eneo ulipo mradi wa maji kijjini hapo.
Kwa taarifa kamili BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...