Taasisi ya Karimjee Jivanje (KJF) imeongeza nguvu zaidi katika kuhifadhi na kusimamia mazingira ya bara la Afrika kwa kudhamini wanafunzi kutoka Tanzania kuendelea na masomo yaliyopendekezwa ya shahada ya uzamili katika eneo hilo. 

Mwenyekiti wa heshima wa kundi la makampuni ya Karimjee Jivanjee nchini Tanzania, Hatim Karimjee alisema mpango huo wa masomo uliundwa na taasisi na mpaka sasa imejitolea kudhamini wanafunzi wawili mwaka 2016 na wanne mwaka huu.

 Alisema Taasisi imetoa msaada wa dola 105,000 sawa na ( 236.2Millioni Tzs) mwaka jana ambapo wanafunzi wawili walichukua kozi ya shahada ya uzamili, na mwaka huu wanafunzi wanne wamedhaminiwa na taasisi ambapo imetoa msaada wa dola 210,000 sawa na (472.5 Miilioni Tzs) na ina mpango wa kutoa dola 180,000 sawa na (405Million Tzs) kwa ajili ya kudhamini nafasi za masomo mwaka ujao “Karimjee Jivanjee imefurahi kuzindua nafasi za masomo ya uhifadhi wa mazingira. 

Wanafunzi hawa watajifunza masomo yalipondekezwa ya shahada ya uzamili ya usimamizi wa uhifadhi wa mazingira ya wanyamapori katika bara la Afrika. Tunapenda kushirikiana na chuo kikuu cha Glasgow nchini Scotland na chuo cha Sayansi na Teknolojia cha Nelson Mandela kilichopo Arusha kuanzisha masomo ya shahada ya uzamili ambapo wanafunzi watasoma mwaka mmoja Glasgow na mwaka mmoja Mkoani Arusha. Wanafunzi hao watatambulika kama wanafunzi kutoka Karimjee,” 
Mwenyekiti wa kundi la makampuni ya Karimjee Jivanjee, Hatim Karimjee (kulia) akimkabidhi kifaa cha kusomea mmoja wa mwanafunzi aliyepata udhamini wa kusoma shahada ya uzamili katika uhifadhi wa mazingira ya wanyamapori katika bara la Afrika Zabibu Kabalika (kushoto) katika hafla iliyofanyika mkoani Arusha. 
Mwenyekiti wa kundi la makampuni ya Karimjee Jivanjee akizungumza wakati wa hafla fupi ya kuzindua masomo yaliyopendekezwa ya kozi ya uzamili katika uhifadhi wa mazingira ya wanyamapori mkoani Arusha, Nyuma Kulia ni Dr. Haydon wa chuo kikuu Glasgow kilichopo Scotland, akifuatiwa na Prof, Karoli Njau wa chuo cha sayansi na teknolojia cha Nelson Mandela, wengine ni wanafunzi waliopata nafasi ya masomo, Zabibu Kabalika (wa tatu kulia) na Evaline Munisi. 
Mwenyekiti wa Kundi la makampuni ya Karimjee Jivanjee akizungumza wakati wa hafla fupi ya kuzindua kozi ya uzamili iliyopendekezwa katika uhifadhi wa mazingira ya wanyamapori mkoani Arusha. kulia ni wanafunzi waliopata nafasi ya masomo ya shahada ya uzamili katika uhifadhi wa mazingira ya wanyamapori Evaline Munisi ( kwanza kulia) na Zabibu Kabalika.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...