Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan
amezitaka Taasisi za Maendeleo ya Fedha za Jumuiya ya Maendeleo Kusini
mwa Afrika (SADC) kuimarisha ushirikiano na kubadilisha uzoefu katika
utendaji wao wa kazi ili kuhakikisha kazi zinazofanywa na Taasisi hizo
zinakuwa na manufaa kwa wananchi wa Jumuiya hiyo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan ametoa kauli hiyo wakati anafungua Mkutano wa mwaka wa Taasisi za Maendeleo ya Fedha za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kwenye ukumbi wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan amesema kuwa kama taasisi hizo za kifedha zitafanya kazi kwa kuzingatia ubunifu na uaminifu ana uhakika kuwa malengo waliyojiwekeza yatafikiwa kwa wakati hasa katika uwekezaji katika miradi mbalimbali ya maendeleo.
Ameeleza kuwa bado upo umuhimu mkubwa kwa Taasisi hizo za Kifedha katika nchi za SADC kuendelea kutumia ipasavyo wataalamu wa vyuo vikuu na taasisi za utafiti kwa lengo la kukuza uchumi unaotokana na ujuzi kupitia ubunifu.
Makamu wa Rais pia amehimiza nchi wanachama wa SADC kupitia taasisi za kifedha za nchi hizo kushirikiana katika kuchangia fedha katika utekelezaji wa miradi mikubwa ya maendeleo katika nchi wanachama wa jumuiya hiyo.
Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dkt Ashatu Kijaji amesema anaimani kubwa kuwa mkutano utasaidia kwa kiasi kikubwa uimarishaji wa utendaji wa kazi katika Taasisi hizo za Maendeleo ya Fedha katika nchi za SADC.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan akiteta jambo na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dkt Ashatu Kijaji.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...