Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akimuangalia mhamiaji haramu katika dirisha dogo la chumba cha mahabusu, Kituo cha Polisi Pangani mkoani Tanga. Mhamiaji huyo kutoka nchini Somalia alikamatwa wilayani Pangani katika mwambao wa Bahari ya Hindi. Masauni akiwa mjini Tanga aliwaagiza Maafisa Uhamiaji na Polisi kuongeza kasi ya kutafuta mizizi ya wahamiaji haramu mkoani humo. Kulia ni Mkuu wa Kituo Polisi mjini Pangani, Christina Musyani. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kulia) akimsikiliza Mkuu wa Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Pangani, mkoani Tanga, Christina Musyani wakati alipokua anamfafanulia masuala ya ulinzi na usalama wilayani humo. Masauni alikikagua kituo hicho pamoja na nyumba za askari polisi ambazo zipo katika hali mbaya zaidi kutokana na kutofanyiwa matengenezo kwa muda mrefu. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (wapili kulia) akimsikiliza Mkuu wa Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Pangani, mkoani Tanga, Christina Musyani alipokuwa anamuonyesha moja ya nyumba ambazo zipo katika hali mbaya zaidi kutokana na kutofanyiwa matengenezo kwa muda mrefu. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akitoka kulikagua Gereza la Wilaya ya Pangani mkoani Tanga. Masauni pia alizungumza na mahabusu wa Gereza hilo kwa kusikiliza kero zao na kuzitolea maamuzi hapo hapo na baadhi kuahidi kuzifanyia kazi kwa haraka zaidi. Kwa nyuma ni Mkuu wa Gereza hilo, Elishinikizo Moshi. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...