Naibu Waziri wa Mambo ya
Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (wapili kulia), Kamishna Jenerali wa
Uhamiaji (CGI), Dkt. Anna Makakala (kulia) wakipokea moja ya kompyuta kutoka
kwa Balozi wa China nchini, Dk. LU Youqing (wapili kushoto) katika hafla ya
makabidhiano ya vifaa msaada vya Tehama vyenye thamani ya shilingi milioni 33
vilivyotolewa na Ubalozi huo kwaajili ya kukisaidia Chuo cha Uhamiaji cha
Kikanda (TRITA) kilichopo mjini Moshi. Kushoto ni Mkuu wa Chuo hicho, Maurice
Kitinusa. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Naibu Waziri wa Wizara ya
Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (wapili kulia-waliosimama) akishuhudia
Balozi wa China nchini, Dk. LU Youqing (kushoto) na Kamishna Jenerali wa
Uhamiaji (CGI), Dkt. Anna Makakala walipokua wakitia saini Mkataba wa
Makabidhiano wa msaada wa vifaa vya Tehama vilivyotolewa na Serikali ya China
kwa ajili ya Chuo cha Uhamiaji cha Kikanda (TRITA), kilichopo mjini Moshi. Picha
na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Naibu Waziri wa Mambo
ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (wapili kushoto), Kamishna Jenerali wa
Uhamiaji (CGI), Dkt. Anna Makakala (kushoto), Balozi wa China nchini, Dk. LU
Youqing (aliyevaa saa) pamoja na maafisa wengine wakimsikiliza Mkuu wa Kitengo
cha Tehama, Chuo cha Uhamiaji cha Kikanda (TRITA), Mkaguzi wa Uhamiaji, Zawadi
Chazuka alipokua anawaonyesha kifaa cha kuangalia alama au maandishi ambayo
hayawezi onekana kwa macho ya kawaida mpaka kifaa hicho kitumike. Ubalozi wa
China ulitoa msaada wa vifaa vya Tehama vyenye thamani ya shilingi milioni 33
kwa ajili ya matumizi ya chuo hicho kilichopo mjini Moshi
Naibu Waziri wa Mambo ya
Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (katikati waliokaa), Kamishna Jenerali wa
Uhamiaji (CGI), Dkt. Anna Makakala (watatu kushoto), Balozi wa China nchini,
Dk. LU Youqing (watatu kulia), Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Wilbroad
Mtafungwa wakiwa katika picha ya pamoja na maafisa Uhamiaji na Ujumbe kutoka
China mara baada ya Balozi wa China kutoa msaada wa vifaa vya Tehama kwa ajili
ya matumizi ya Chuo cha Uhamiaji cha Kikanda (TRITA) kilichopo mjini Moshi. Picha
zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Naibu Waziri wa Mambo
ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kulia) akipokelewa na Kamishna
Jenerali wa Uhamiaji (CGI), Dkt. Anna Makakala, wakati kiongozi huyo alipokua
anawasili Chuo cha Uhamiaji cha Kikanda (TRITA), mjini Moshi kwa ajili ya kukabidhiwa
vifaa vya Tehama vilivyotolewa na Ubalozi wa China nchini kwa ajili ya matumizi
ya chuo hicho.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...