Mbunge wa Viti Maalumu Mhe. Lucy Mayenga jana alikabidhi gari la wagonjwa Mkuu wa wilaya Shinyanga mjini Mhe. Josephine Matiro katika sherehe fupi iliyofanyika mjini humo. Sambamba na gari hilo pia Mhe. Mayenga alitoa Shilingi milioni 17 ambapo milioni 15 ni mchango wake wa ujenzi wa chumba cha upasuaji na milioni mbili kwa ajili ya kifaa cha maabara katika kituo cha Afya cha Kambarage.
Mbunge wa Viti Maalumu Mhe. Lucy Mayenga akionesha funguo la gari la wagonjwa kabla ya kuikabidhi kwa Mkuu wa wilaya Shinyanga mjini Mhe. Josephine Matiro (kulia) katika sherehe fupi iliyofanyika mjini humo
Mbunge wa Viti Maalumu Mhe. Lucy Mayenga akisindikizwa kwa nderemo na wananchi waliojawa na furaha baada ya kukabidhi gari la wagonjwa kwa Mkuu wa wilaya Shinyanga mjini Mhe. Josephine Matiro (kulia) katika sherehe fupi iliyofanyika mjini humo
La wagonjwa ambalo Mbunge wa Viti Maalumu Mhe. Lucy Mayenga amemkabidhi Mkuu wa wilaya Shinyanga mjini Mhe. Josephine Matiro.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...