Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Mh. Isaya Mwita akizungumza na Meneja Masoko na Mawasiliano wa Mfuko wa Pensheni wa Serikali za Mitaa LAPF Bw. James Mlowe wakati alipotembelea katika banda la Mfuko wa Pensheni wa LAPF kwenye viwanja vya maonyesho ya biashara vya Mwalimu J.K. Nyerere Barabara ya Kilwa jijini Dar es salaam.

Mfuko wa LAPF na Jiji la Dar es salaam wana Mpango kabambe wa kutekeleza ujenzi wa kituo kipya cha mabasi ya kwenda mikoani jijini Dar es salaam utakaogharimu zaidi ya shilingi Bilioni 30.
Meneja Masoko na Mawasiliano wa Mfuko wa Pensheni wa Serikali za Mitaa LAPF Bw. James Mlowe akitoa maelezo kwa Meya wa Jiji na Meya wa Kinondoni Mh. Benjamin Sitta wakati mameya hao walipotembelea katika banda la mfuko huo leo
Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Mh. Isaya Mwita na Meya wa Kinondoni Mh. Benjamin Sitta wakisaini kitabu cha wageni wakati walipowasili katika banda hilo kulia ni Meneja Masoko na Mawasiliano wa Mfuko wa Pensheni wa Serikali za Mitaa LAPF Bw. James Mlowe.
Matukio mbalimbali ya picha yakiontesha baadhi ya wafanyakazi wa LAPF wakiwahudumia wananchi waliofika kwenye banda la mfuko wa Pensheni wa LAPF kwenye Maonyesho ya Sabasaba barabara ya Kilwa leo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...