Mwenyekiti wa kampuni ya Upimaji na Upangaji wa Makazi (HUSEA), Renny Chiwa akitoa maelezo machache juu ya mradi wa 'Ardhi Clinic' katika uzinduzi wa uliofanyika Kata ya Msigani-Mbezi wilaya ya Ubungo jijini Dar es Salaam. Bw. Chiwa alisema kuwa lengo la mradi huo ni kusaidia juhudi za serikali za kupanga, kupima na kumilikisha kila kipande cha ardhi nchini nzima na pia kuboresha maisha ya mamilioni ya watanzania kupitia ushauri na utoaji elimu kwa wananchi katika masuala yote ya ardhu kwa nia ya kutengeneza makazi bora yaliyopangwa na kupimwa kwa ajili ya kizazi cha sasa na baadae.
Mkurugenzi wa kampuni ya Upimaji na Upangaji wa Makazi (HUSEA), Pamela Maro akiwafafanua machache mbele ya waandishi wa habari juu ya Mradi wa 'Ardhi Clinic' katika uzinduzi uliofanyika katika Kata ya Msigani, Mbezi jijini Dar es Salaam. Alisema kuwa malengo makuu ya mradi wa 'Ardhi Clinic' ni tiba mbadala kwa changamoto mbali mbali za masuala ya ardhi baada ya kugundua kuwa changamoto nyingi zinatokana na masuala ua ardhi hapa Tanzania kama migogoro ya wafugaji na wakulima, wananchi kuuziwa maeneo ya wazi, utapelikwenye masuala ya ardhi, uendelezaji wa makazi usiofuata mipango, ukosefu wa maadili katika taaluma za upangaji na upimaji, ukosefu wa hati miliki, ukosefu wa huduma za jamii n.k hazina tofauti na magonjwa ambayo wanahitaji tiba haraka kuyakabili.
Wananchi wakiendelea kupata elimu ya ardhi. 
Vifaa vya kisasa vinavyotumika katika upimaji wa ardhi. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...