Na Judith Mhina - MAELEZO

Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Rais wa Kwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni muasisi aliyeenzi lugha adhimu na tamu ya Kiswahili na anastahili tuzo maalum kwa kutambua umuhimu wa lugha  hiyo katika kuleta umoja, mshikamano, na maendeleo barani Afrika.

Mwalimu kwa kutambua umuhimu wa lugha ya Kiswahili, alianza kuweka mfumo wa matumizi ya lugha hiyo katika utendaji wa serikali, jamii nzima ya Tanzania na Umoja wa Afrika. Aidha, sera za Tanzania za kushiriki katika kupigania Uhuru wa nchi kadhaa za Afrika na uwepo wa wakimbizi nchini kwa idadi kubwa imewezesha lugha hii kuvuka mipaka na kuenea kote kusini mwa Afrika.

Mwalimu amepata wapiganaji mahiri wa lugha ya Kiswahili ambao wapo wengi, lakini kwa uchache makala yangu itaangazia viongozi yaani, Rais mstaafu wa Awamu ya Pili, Mzee Ali Hassan Mwinyi, na Rais mstaafu wa Msumbiji Joachim Chissano, Marais wa Uganda Yoweri Kaguta Museveni, Rwanda, Paul Kagame, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Joseph Kabila na Jemedari wa kuenzi lugha ya Kiswahili anayeifanya lugha hii kuwa Lulu, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli. 

Mtakubaliana nami mchango wa Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi katika kutumia lugha ya Kiswahili fasaha, katika shughuli zote za Serikali na za kijamii zilisukuma mwamko wa gurudumu la kiswahili kusonga mbele haswa kwa wale wanaodhani lugha za kigeni ni bora kuliko lugha yao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...