Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu akikata Utepe kuashiria uzinduzi wa bima ya afya ya Mtoto 'Toto Kadi' leo katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.

Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu amesema kuwa kiu yake katika sekta ya afya ni kuona kila mtu ana bima ya afya.

Waziri Ummy ameyasema hayo leo wakati wa uzinduzi wa Kadi ya Bima ya Afya kwa Mtoto ‘Toto Kadi’ , amesema kuwa taifa kuwa lina maendeleo linatokana na msingi wa afya  ambapo msingi huo unatokana  na kuwa watoto wanaopata huduma za afya kwa uhakika.

Amesema kuwa  gharama za kulipa matibabu katika ukuaji watoto na hali uchumi  ni kubwa lakini kuwepo kwa bima hiyo kutanya wazazi kuwa na  furaha wakati wote hata ikitokea ugonjwa bima ndio inamaliza matatizo.
Ummy amesema kuwa wakati  anaingia madarakani alikutana na Rais Dk. John Pombe  Magufuli  alichoendanacho ilikuwa ni kuongeza ghrarama lakini Rais alisema hakuna kuongeza ghrama yeyote cha msingi waangalie jinsi ya kusaidia watanzania kuwa na bima.

Aidha Waziri  Ummy amewaomba Mfuko wa  Taifa wa Bima ya Afya (NHIF)  kuja na bima ya mama mjamzito itakayotumika wakati ujauzito na badaa ya kujifungua.

Ummy amesema kuwa kampeni hiyo iwe endelevu kwa nchi nzima ili watoto wote kuwa na bima ya afya hapo tutakuwa tunajenga taifa lenye msingi bora wa afya.Waziri  huyo ameitaka kuweka utaratibu wa kubandika mabango katika kila kumbi za starehe ili wanavyotumia vinywaji waweze kuangalia watoto kama wana kadi ya afya bima ya afya.

Nae Mwenyekiti wa Bodi NHIF, Anne Makinda amesema kuwa wanafanya kazi nguvu kuhakikisha watanzania wanapata huduma za afya  pamoja na kulipa watu wanaotoa huduma kwa bima ya afya.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu akiangalia muundo wa kadi ya bima ya afya ya Mtoto mara baada ya kuzindua leo katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu akipeana Mkono na Mwenyekiti wa Bodi wa NHIF, Anne Makinda  mara baada ya kuzindua bima  kadi ya bima ya afya kwa watoto leo katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu akizungumza katika uzinduzi wa bima ya afya kwa mtoto katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa NHIF, Bernad Konga akizungumza juu ya mpango wa bima ya afya ya Mtoto katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akizungumza juu ya bima ya afya kwa mtoto katika jiji la Dar es Salaam wakati uzinduzi wa bima hiyo katika viwanja vya mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.

BOFYA HAPA KUONA PICHA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...