Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) lazindua utoaji wa mikopo kwa SACCOS
na kupitia Benki ya Azania. Mikopo hii ni mahususi kwa ajili ya kuwasaidia wanachama
wa NSSF kuweza kujikwamua kiuchumi hususan kuweza kutekeleza sera ya Viwanda
ya awamu ya tano kwa kutumia mikopo hiyo kufungua Viwanda vidogo vidogo.
Mikopo
hiyo itatolewa hadi kiwango cha juu kisichozidi fedha taslimu za kitanzania 300,000,000
kwa SACCOS au AMCOS. Vile vile mwanachama wa NSSF anaweza kukopa hadi
shilingi 20,000,000 kupitia SACCOS au AMCOS aliyojiunga nayo na mikopo hiyo
italipwa ndani ya miezi 24.
Alipokuwa akizindua mpango huo, Makamu wa Rais Mhe. Mama Samia Suluhu Hassan
aliwaasa wanachama wa NSSF kuchangamkia fursa hiyo ya mikopo na kuwaomba
waitumie mikopo hiyo kama chachu ya kujikwamua kiuchumi na kuwaasa kuwa na
nidhamu ya hali ya juu katika kuendeleza biashara zao.
Akizungumza na waandishi wa Habari wakati wa uzinduzi wa mpango huo Mkurugenzi
Mkuu wa NSSF Prof Godius Kahyarara alisema SACCOS na AMCOS zote
zitakaoomba mikopo hiyo ni lazima ziwasilishe taarifa sahihi za fedha zilizokaguliwa
kwa miaka mitatu na kuhakikiwa na COASCO na mwanachama anaruhusiwa kukopa
hadi mara tatu ya Amana zake alizijiwekea ndani ya SACCOS au AMCOS ambayo
yeye ni mwanachama.
Makamu wa Rais wa Jammhuri ya muungano wa Tanzania Mhe. Mama Samia Suluhu Hassan akikata
utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa Mikopo ya Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) Kupitia Benki ya Azania alipotembelea banda la NSSF
katika maonesho ya Sabasaba katika viwanja vya Mwalimu Nyerere.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mama Samia Suluhu Hassan akipata
maelezo kuhusu dawa ya kuangamiza viuadudu vinavyosababisha ugonjwa wa malaria alipotembelea
banda la Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) katika maonesho ya Sabasaba, viwanja vya Mwalimu Nyerere. NSSF ni mdau wa kiwanda
hicho cha Viuadudu kilichopo mkoani Pwani.
Mkurugenzi mkuu wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Prof. Godius Kahyarara akitoa ufafanuzi kuhusu mikopo ya NSSF kwa Makamu wa Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Mhe Mama Samia Suluhu Hassan kabla ya kuzindua rasmi mikopo hiyo katika viwanja vya Sabasaba.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...